MMILIKI WA MABASI YA HBS NA SABENA AJIUA KWA KUJIPIGA RISASI

Mfanyabiashara Sultan Ahmed au maarufu Chapa ambaye ni mmiliki wa Kampuni ya mabasi ya HBS na Sabena anadaiwa kujiua kwa kujipiga risasi ambayo iliingilia mdomoni kisha kutokea kisogoni leo Jumatano Aprili 11,2018 majira ya saa tatu asubuhi.
Taarifa za tukio hilo zinadai kwamba, Sultanambaye ni mwenye asili ya Kiarabu pía ni mmiliki wa kituo kikubwa cha uuzaji wa mafuta ya petroli wilayani Sikonge amejipiga risasi akiwa nyumbani kwake wilayani Sikonge mkoani Tabora huku chanzo cha uamuzi huo wa kujitwanga risasi kikiwa hakijajulikana.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora SACP Wilbroad Mutafungwa amethibitisha tukio hilo na kwamba wanafanya uchunguzi juu ya mauaji hayo.

Comments

Popular posts from this blog