Uchangudoa wa Zari Waibua Kimbembe!


MAMBO ni moto! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya mfanyabiashara maarufu Afrika Mashariki, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kukiri kuwa yeye ni changudoa mzee, kauli yake imeibua kimbembe.

KUPITIA SNAPCHAT
Kupitia mtandao wake wa kijamii wa Snapchat, mwishoni mwa wiki iliyopita, Zari alitupia ujumbe akionesha kuwa yeye ni changudoa mzee, lakini mwenye mafanikio akimjibu hasimu wake, mwanamitindo Hamisa Mobeto bila kumtaja. “Bora mimi changudoa mzee niliye na mafanikio na bado ananipenda kuliko kijana wa miaka 20+, mama uliyeachwa mara mbili na tuzo juu,” alisema Zari kupitia Snapchat. Kwa muda mrefu, Zari amekuwa kwenye tifu la aina yake baada ya Mobeto kuzaa na bwana wake, msanii wa Bongo Fleva miezi michache iliyopita.

KIBEMBE KILIVYOIBUKA
Kitendo cha Zari kutoa kauli hiyo, kimbembe kiliibuka mtandaoni mara baada ya ukurasa wa Instagram wa Global Publisher, kutupia habari hiyo ambapo wafausi wa mtandao huo walianza kurushiana maneno makali huku kila mmoja akitoa msimamo wake.


AUNGWA MKONO, AKOSOLEWA
Kuna ambao waliunga mkono kauli hiyo kwa kile walichosema kwamba aliandika kwa maana ya kumkejeli Mobeto, lakini si kwamba ni kweli yeye ni changudoa, lakini wengine walicharuka na kusema kweli yeye ni changudoa. “Jamani Zari siyo changudoa acheni kumshambulia kwa matusi. Yule amesema vile kama kumkejeli Mobeto ambaye aliingia kwenye anga zake, watu wengine sijui mkoje, mmekalia ujingaujinga tu,” alichangia shabiki mmoja mtandaoni akimkingia kifua Zari.
Baada ya shabiki huyo kumtetea Zari, wengine waliibuka na kumshambulia mama huyo wa watoto watano kwa kile walichosema kwamba kweli mrembo huyo wa Uganda ni changudoa aliyejivisha ‘ngozi’ ya ustarabu. “Acheni mambo ya kipuuzi…hivi mnafikiri Zari ana hela kama inavyodaiwa? Yule ni changuduoa tu kama walivyo machangu wengine na kama yeye mwenyewe alivyosema. Sema kinachompa hadhi yeye anajiuza kwa staha tofauti na wenzake wanaojipanga barabarani.

UTAJIRI WAKE WAHUSISHWA
“Kule Sauz (Afrika Kusini) mnavyoona anaishi kwenye majumba ya kifahari, anavyoonekana ana magari mapya kila siku mnafikiri yale ni jasho lake? Uchangudoa tu ule ndiyo unaompa utajiri wote alionao, yule msanii anajiona amepata kumbe amepatikana,” alisema shabiki huyo.
Mvutano huo ambao hadi tunakwenda mitamboni ulikuwa ukiendelea kwenye ukurasa huo wa Global Publishers unaaongoza kwa kutembelewa na watu wengi ndani na nje ya Bongo, ulisababisha watu kurushiana matusi ya nguoni huku wengine wakienda mbali kwa kutaka kutafutana uso kwa uso, nje ya mtandao huo wa Instagram ili wapeane ngumi kavukavu.

MWENYEWE AANIKA UKWELI
Baada ya kauli hiyo kuibua kimbembe, Zari amekuwa amewatolea uvivu kwa kuonesha namna ambavyo ni mchapakazi kupitia ofisi zake mbalimbali zinazomuingizia kipato halali tofauti na watu wanavyofikiri na kuweka mawazo yao kwenye mitandao ya kijamii.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Zari amekuwa akionesha picha za maduka yake ya nguo yaliyopo Afrika Kusini kwa kusindikiza na meseji mbalimbali zinazoashiria kwamba yeye si mtu wa mchezomchezo linapokuja suala la uwajibikaji. Ameonesha kwamba anatenga muda wake kwa kuwa bize na kazi, lakini pia anatenga muda wake kwa ajili ya kufurahia maisha kwa maana ya kuponda starehe katika viunga mbalimbali pande za Sauz na nyumbani kwao, Uganda.

ANA VYUO SAUZ
Kama hiyo haitoshi, kupitia mahojiano yake ambayo yapo kwenye mtandao wa Kijamii wa You Tube, Zari alifunguka kuwa anavyo vyuo vya urembo na masuala ya ulinzi. Pamoja na hayo, amekuwa amekuwa akizungumzia mafanikio mbalimbali anayoyapata kupitia matamasha yake makubwa hususan lile la Zari All White Party ambalo linampa mkwanja mrefu kila mwaka.
STORI: Erick Evarist, Dar IJUMAA WIKIENDA

Comments

Popular posts from this blog