
Polisi wakiimarisha ulinzi eneo hilo.
MTAA wa Jacaranda jijini Nairobi, Kenya, leo umefungwa na polisi ili
kuzuia mkutano wa umoja wa vyama vya upinzani nchini humo, National
Super Alliance (NASA) uliopangwa kwa ajili ya kuwakumbuka wafuasi wake
27 waliouawa wakati wa maandamano ya kupinga uchaguzi wa marudio
uliofanyika zaidi ya wiki moja iliyopita.

Mataili yakiwa yamechomwa moto.
Mkutano huo ulipangwa kufanyika leo ambapo Rais Uhuru Kenyatta
ameapishwa kwa kipindi cha pili katika uwanja wa michezo wa Kasarani.
Chumba vya kutunzia maiti katika jiji hilo pia kimefungwa na polisi
ambapo watu hawatakiwi kufika hapo.

Hali ilivyokuwa eneo la tukio.
Polisi waliokuwa na zana zote za kuzuia fujo wamekuwa wakirusha
mabomu ya machozi sehemu nyingi yakiwemo maeneo ya wafuasi wa NASA ambao
wamefunga barabara kadhaa jijini humo.

Wafuasi wa NASA wakipambana na polisi.
Mpinzani mkuu nchini humo, Raila
Odinga, amepinga mipango ya kumwapisha katika nafasi ya urais, akisema
hilo linaweza kuleta vurugu na vifo zaidi.

Mataili yakiwa yamechomwa moto.
Aliyasema hayo akionyesha mifano ya nchi za Ivory Coast na Gambia
ambazo zilifanya hivyo kutokana na migogoro ya uchaguzi na hivyo
kuwaapisha Alassane Quatara na Adama Barrow, hali aliyosema si sawa na
ile iliyotokea nchini Kenya.
Pamoja na kuzuiwa kwa mkutano huo wa upinzani, inasemekana polisi
wamepiga kambi karibu na makazi ya viongozi wa NASA, akiwemo Mbunge wa
Dagoretti Kaskazini, Simba Arati.
Comments
Post a Comment