Amtosa Mumewe Ulaya, Achukuliwa na Kiserengeti cha Gambia
Mama mwenye watoto tisa Heidi Hepworth (44) akiwa na mpenzi wake wa sasa Mamadou Jallow.
MWANAUME mmoja mkazi wa Uingereza Andy Hepworth, amesimulia kwa huzuni jinsi mkewe Heidi Hepworth (44) alivyomtosa, akamwachia watoto tisa na hivi sasa anajirusha na kivulana cha kutoka Gambia, Afrika.
Mwanamke huyo anaishi na kijana huyo anayejulikana kama Mamadou Jallow (30) baada ya kufahamiana kupitia Mtandao wa Facebook ambapo aliamua kumfuata hukohuko Gambia na mpaka sasa anaishi naye huko.
Jinsi alivyokolewa na mapenzi hayo mapya, sasa Heidi anadai talaka na kusema kuwa amempata ampendaye zaidi.
…Enzi ya ndoa yao na mume wake Andy.
Hivi sasa ni kama shetani ameukamata mwili wake. Kijana aliyenaye ameivuruga akili yake ambapo na yeye anafuata kila kitu.” Heidi naye anasema: “Nimekutana na kijana mpya, jambo ambalo si la kushangaza.
…Akiwa na mume wake Andy.
Afukuza ambapo mimi na yeye tulizaa watoto tisa.” Anaongeza kwamba alianza kuyaona mabadiliko kwa mkewe huyo tangu Machi mwaka huu baada ya kugundua majina ya marafiki wa kiume kutoka Afrika na Asia kwenye kompyuta yao ya nyumbani na alipomwuliza alikana.
Hivi sasa Heidi na Mamadou wanaishi jijini Banjul na mama huyo amekanusha kwamba anatumiwa na kijana huyo ili apate pasipoti ya kuingia Uingereza. “Hilo halipo kabisa, nimempenda, basi! Hakuna mwingine. Kuhusu watoto, bado nawakumbuka sana. Sidhani kama nitaondoka hapa, lakini watoto wangu bado nawakumbuka,” alisema Heidi.
Comments
Post a Comment