Wolper atoa onyo hili kali


MUIGIZAJI mwenye jina Bongo, Jacqueline Wolper ‘Wolper’ amefunguka kuwa kuna watu wamekuwa wakipiga pesa kwenye mitandao ya kijamiii kwa njia mbalimbali kupitia jina lake jambo ambalo hapendezwi nalo.

Akichonga na Uwazi Showbiz, Wolper aliongeza kuwa taarifa juu ya watu hao anazo na anazifanyia kazi, upelelezi wake ukikamilika atawafikisha kwenye vyombo husika ili wakacheze na mkono wa sheria.

“Kuna watu mitandaoni wanapiga pesa kupitia jina langu kwa njia mbalimbali ambazo nimeshazifahamu. Sasa mimi nawaonya tu na kuwataka waache mara moja maana dawa yao inachemka jikoni,” alisema Wolper.

Comments

Popular posts from this blog