TEKNOLOJIA MPYA KUOKOA MAZAO YANAYOPOTEA




mkulima alizeti4 
Na Mahmoud Ahmad,Arusha.
Uhifadhi duni na mbovu wa mazao husababisha wakulima kupoteza aslimia 5%ya mazao yao  kuanzia shambani kabla ya kuvunwa na kusafirishwa hadi kwenye masoko
Hayo yameelezwa na Msimamizi wa kituo cha kueneza teknolojia ya kilimo kanda ya kaskazini (ATTC)  Ernest Elias alipokuwa akizungumzia teknolojia mpya ya mavuno  ambayo wanayoonyesha katika maonyesho ya nane nane mwaka huu yanayofanyika katika viwanja vya Taso vilivyoko kata ya themi jijini hapa
Ernest Elias amesema kuwa teknolojia hiyo mpya ambayo wameionyesha kwa mara ya kwanza katika maonyesho hayo itawasaidia wakulima kuvuna kwa urahisi na kufungasha wakiwa huko huko shambani kwa namna ambayo haitaruhusu upotevu wa mazao hata wakati wa usafirishaji na masokoni pia.
Elias alisema kwa wastani  Mkulima akivuna gunia 10 anapoteza gunia 1 kutokana na  ubovu wa uhifadhi  wa mazao na mfumo mzima hadi kumfikia mhitaji sokoni.
Msimamizi huyo amesema kuwa upotevu wa mazao licha ya kupunguza mazao ya mkulima pia kuna mfanya mkulima kubeba mzigo mkubwa wa gharama za uzalishaji ambao ungeweza kubebwa na mazao yaliyopotea hivyo kuzibwa kwa mianya ya upotevu wa mazao ya wakulima kutawasaidia wakulima.
Pia amewaasa wakulima watumie teknolojia za kisasa zitakazowasaidia kupunguza gharama za uzalishaji na kuwasaidia kufanya kilimo chenye tija.

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI




“PRESS RELEASE” TAREHE 06. 08. 2013.

WILAYA YA ILEJE - MAUAJI

MNAMO TAREHE 05/08/2013 MAJIRA YA SAA 17:00 HUKO KIJIJI CHA IBABA WILAYA YA ILEJE NA MKOA WA MBEYA. MTOTO JOSHUA S/O MWAMPAMBA ,4YRS , MNDALI NA MKAZI WA KIJIJI CHA IBABA ALIUAWA KWA KUPIGWA NGUMI NA MATEKE SEHEMU MBALIMBALI ZA MWILI  WAKE NA MIKA S/O KISUNGA ,20YRS, MNDALI NA MKAZI WA KIJIJI CHA IBABA. MTUHUMIWA AMEKAMATWA PAMOJA NA KUWA NA MATATIZO YA AKILI, MWILI WA MAREHEMU UMEFANYIWA UCHUNGUZI NA   DAKTARI WA SERIKALI NA KUKABIDHIWA KWA NDUGU KWA MAZISHI. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANATOA WITO KWA JAMII KUWA NA UANGALIZI MAALUMU KWA WATU WENYE MATATIZO YA AKILI ILI KUEPUSHA MADHARA YANAYOWEZA KUJITOKEZA .

WILAYA YA CHUNYA – KUJERUHI

MNAMO TAREHE 05/08/2013 MAJIRA YA SAA 24:30 HRS HUKO KIJIJI CHA MWAMBANI WILAYA YA CHUNYA MKOA WA MBEYA. DAFROSA D/O SAIDIA, 30YRS MNYAMWANGA, MKULIMA ALICHOMWA KISU UPANDE WA KULIA WA TUMBO NA UTUMBO KUTOKA NJE NA MTUHUMIWA AMBAYE NI MPENZI WAKE ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA  NJELE S/O LUHENDE ,MKAZI WA MWAMBANI. CHANZO CHA TUKIO HILO NI WIVU WA KIMAPENZI BAADA YA MTUHUMIWA KUMKUTA MHANGA AKIWA AMEKAA BAA NA MWANAUME MWINGINE. MTUHUMIWA ALITOROKA MARA BAADA YA TUKIO HILO NA MAJERUHI AMELAZWA HOSPITALI TEULE YA MWAMBANI CHUNYA. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANATOA WITO KWA JAMII KUTATUA MATATIZO/MIGOGORO YAO YA KIJAMII KWA NJIA YA MAZUNGUMZO ILI KUJIEPUSHA NA MATATIZO YANAYOWEZA KUJITOKEZA.

WILAYA YA CHUNYA – KUPATIKANA NA POMBE HARAMU YA MOSHI [GONGO]

MNAMO TAREHE 05.08.2013 MAJIRA YA SAA 14:00HRS HUKO ENEO LA KALUNGU KIJIJI CHA MAKONGOLOSI WILAYA YA CHUNYA NA MKOA WA MBEYA.  ASKARI POLISI WAKIWA DORIA WALIMKAMATA ANNA D/O MWAKALINGA ,30 YRS,KYUSA,MKULIMA NA MKAZI WA KALUNGU  AKIWA NA POMBE HARAMU YA  MOSHI [GONGO] UJAZO WA LITA 15.  MTUHUMIWA NI MUUZAJI WA POMBE HIYO TARATIBU ZA KUMFIKISHA MAHAKAMANI ZINAFANYWA. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI  ANATOA WITO KWA JAMII KUACHA KUTUMIA POMBE HARAMU YA MOSHI [GONGO] KWANI NI KINYUME CHA SHERIA SAMBAMBA NA KUWA NI HATARI KWA AFYA YA MTUMIAJI.

WILAYA YA CHUNYA – KUPATIKANA NA SILAHA

MNAMO TAREHE 05.08.2013 MAJIRA YA SAA 12:30 HRS HUKO KIJIJI CHA ISANZU WILAYA YA CHUNYA NA MKOA WA MBEYA. ASKARI POLISI WAKIWA DORIA WALIMKAMATA JACKSON S/O LAIN, 61YRS, MNYIHA, MKULIMA NA MKAZI WA ISANZU AKIWA NA BUNDUKI AINA YA GOBOLE .MBINU NI KUFICHA SILAHA HIYO JUU YA DARI NDANI YA NYUMBA YAKE. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI  ANATOA WITO KWA JAMII KUACHA MARA MOJA TABIA YA KUMILIKI SILAHA BILA KIBALI KWANI NI KINYUME CHA SHERIA NA NI KOSA LA JINAI.


WILAYA YA RUNGWE - KUPATIKANA NA BHANGI

MNAMO TAREHE 05.08.2013 MAJIRA YA SAA 14:00HRS HUKO ENEO LA KK WILAYA YA RUNGWE MKOA WA MBEYA.  ASKARI POLISI WAKIWA DORIA WALIWAKAMATA WATUHUMIWA WATANO [5]  AMBAO NI  [1] MAJALIWA  S/O HERIOT, 21 YRS,KYUSA, MKULIMA NA MKAZI WA KK, [2] RAMADHANI S/O MAJID ,25 YRS , MPERE,MWANAFUNZI WA SEKONDARI NA MKAZI WA KK,[3] IMANI S/O ALLY ,22YRS,KYUSA,MKULIMA WA KK TUKUYU [4] IPYANA S/O GIDION,23 YRS  KYUSA MKULIMA WA KK NA [5] ISAYA S/O GIDION,21 YRS, KYUSA,MKULIMA WA KK WAKIWA NA MISOKOTO 32, KETE 34, NA GRAMU 7  ZA BHANGI AMBAZO NI SAWA NA UZITO WA GRAMU 337. WATUHUMIWA NI WATUMIAJI NA WAUZAJI WA BHANGI HIYO TARATIBU ZA KUWAFIKISHA MAHAKAMANI ZINAFANYWA. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI  ANATOA WITO KWA JAMII KUACHA KUTUMIA DAWA ZA KULEVYA [BHANGI] KWANI NI KINYUME CHA SHERIA SAMBAMBA NA KUWA NI HATARI KWA AFYA YA MTUMIAJI.

Signed By,
 [DIWANI ATHUMANI   - ACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

MSTUKOO WA HATARI!!!!! HOTELI INAYOUZA NYAMA ZA BINADAMU YAGUNDULIWA











Comments

Popular posts from this blog