Posts

Baada ya Timu ya Taifa ya Chad Kujitoa AFCON 2017, Haya ndio Maamuzi ya CAF......

Image
Jumatatu ya March 28 timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars ilikuwa inajiandaa kushuka dimbani kucheza mchezo wake wa nne wa kuwania kufuzu michuano ya mataifa ya Afrika 2017 dhidi ya Chad, habari zilizotoka March 27 kutoka shirikisho la soka Afrika CAF ni kuwa Chad wamejitoa. Baada ya Chad kujitoa kwa sababu za kutokuwa vizuri kiuchumi, CAF wamekumbushia sheria iliyowekwa January 15 2015, inaeleza kuwa kundi lolote litakalo salia na timu tatu, halitakuwa na best looser na badala yake kinara wa kundi ndio atakuwa anafuzu michuano hiyo pekee. Kwa sheria za CAF michezo ya Chad inafutwa na msimamo wa Kundi G unabakia kuongozwa na Misri kwa point 4, Nigeria point 2 na Tanzania kubakia mkiani kwa kuwa na point moja, ikumbukwe kuwa Taifa Stars ilicheza na Chad March 23 N’Djamena na kufanikiwa kuibuka na ushindi wa goli 1-0.

Penny azimia ndani ya gari, ala mzinga

Image
Muonekano wa gari hilo baada ya kugongwa. Stori:  Imelda Mtema, Wikienda Dar es Salaam: Bidada yamemkuta! Mtangazaji wa Zuku TV, Penniel Mungilwa ‘VJ Penny’ amekumbwa na mkasa mwingine baada ya gari lake kupigwa mzinga maeneo ya Mikocheni jijini Dar, kwa kile kinachodaiwa alizimia barabarani kutokana na tatizo la ini linalomsumbua kwa sasa. Chanzo makini ambacho kilishuhudia tukio hilo kilisema kuwa staa huyo alikuwa akiendesha gari lake aina ya Toyota Mark X kwa mwendo wa kawaida lakini akaanza kupunguza spidi taratatibu kutokana na maumivu yaliyompata ghafla na kusababisha bodaboda kugonga gari lake kwa nyuma. Mashuhuda wakiwa kwenye tukio. Mpashaji wetu aliendelea kusema kuwa, wakati tukio hilo linatokea ilikuwa mchana kweupe bodaboda nusura wamfanyizie. Pamoja na watu kusogelea kwenye tukio, Penny aliendelea kukaa ndani ya gari akiwa amejilaza hadi alipopata nafuu ndipo akaanza kuondoa gari taratibu. Wikienda lilipozungumza na Penny alisema alipatwa na hali hiyo

SAKATA LA RAY C KURUDI KWENYE MADAWA YA KULEVYA JIPYA LAIBUKA,ANASWA LIVE

Image
Stori: Musa Mateja, WikiendaLICHA ya kutumia nguvu nyingi kukanusha habari zinazochapishwa na Magazeti Pendwa ya Global Publishers kuwa, amerejea kwenye matumizi ya madawa ya kulevya ‘unga’, hatimaye staa wa Bongo Fleva, Rehema Chalamila ‘Ray C’ amenaswa ‘laivu’ akiwa ‘ameangusha gari’ kando ya barabara, habari ndiyo hiyo! Ray C ambaye kila anapoandikwa na Magazeti ya Global kuhusu kurejea kwenye unga, amekuwa akimtupia shutuma Mkurugenzi wa Global, Eric Shigongo kwamba anamchafua, alinaswa na mapaparazi wetu hivi karibuni maeneo ya Mwananyamala Magengeni, Dar akiwa amezima yeye na mwanaume aliyekuwa naye hali iliyompa urahisi paparazi wetu kuwafotoa picha za kutosha. ISHU ILIANZA JANUARI Januari mwaka huu, gazeti hili liliripoti habari iliyokuwa na kichwa; CHIMBO LA UNGA LA RAY C LAGUNDULIKA. Baada ya habari hiyo kutoka, Ray C aliikanusha kupitia ukurasa wake wa Instagram akisema: “Seriously kwa kweli huwa naumia sanasana kuona binadamu mwenzangu anadiriki kuniharibia j

RAIS MAGUFULI AHUDHURIA IBADA YA PASAKA KANISA LA KKKT LA AZANIA FRONT JIJINI DAR ES SALAAM

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akilakiwa na Askofu Mkuu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dkt. Alex Malasusa alipowasili kwa Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo Machi 27, 2016. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Mchungaji Charles Mzinga alipowasili kwa Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo Machi 27, 2016. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na Mkewe Mama Magufuli wakishiriki na waumini wengine Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo Machi 27, 2016. Kwaya wakati wa Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo Machi 27, 2016. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimia waumini h

Fahamu aina saba za uvimbe kwenye mayai ya mwanamke

Image
Kuna aina nyingi za uvimbe kwenye mayai ya mwanamke na kusababisha maumivu kwao lakini aina hizi saba ndiyo huonekana sana kwa wanawake wengi ambazo ni kama ifuatavyo:  I. Follicular cyst :  Ni uvimbe ambao hutokea wakati Ovulation isipotokea au baada ya Corpus Luteum kuanza kusinyaa na kupotea yenyewe baada ya kutopachikwa kwa yai kwenye kuta za mfuko wa kizazi. Uvimbe huu unakuwa na wastani wa inchi 2.3 kwa upana. Upasukaji wa uvimbe huu husababisha maumivu makali sana katikati ya mzunguko wa hedhi yaani siku ya Ovulation. Maumivu haya huonekana kwa robo ya wanawake wenye aina hii ya uvimbe. Kwa kawaida, uvimbe huu hauna dalili zozote na hupotea wenyewe baada ya miezi kadhaa. 2.Corpus Luteum cyst ;  Ni uvimbe unaotokana na kutopachikwa kwa yai la uzazi lililorutubishwa na mbegu ya kiume kwenye mfuko wa kizazi. Kwa kawaida Corpus Luteum husinyaa na kupotea yenyewe, au wakati mwingine inaweza ikajaa maji na hivyo kusababisha uvimbe wa aina hii. Uvimbe huu huonekana kwen

Clouds media wamtembelea Chid Benzi Bagamoyo

Image
Wanafamilia wa ‪#‎CloudsMediaGroup‬ kutoka katika vipindi vya ‪#‎PowerBreakFast‬ ‪#‎Clouds360‬ na ‪#‎Harakati‬ wametembelea kituo cha Life &hope Rehabilitation centre "Bagamoyo" mahali ambapo Rapa Chidy Benz anapatiwa matibabu, wameongea na watumiaji sugu wa madawa ya kulevya ambao wanapatiwa matibabu katika kituo hicho kuhusu uzoefu wao hapo. Inategemewa kuwa Chidy Benz itamchukua siku 90 kuondoa madawa katika mwili wake na miezi 6 kumaliza matibabu yake kabisa. Pia wamewatakia sikukuu njema ndugu zetu hao.

Baba Diamond Ashinda Njaa

Image
NA WAANDISHI WETU, Risasi Jumamosi DAR ES SALAAM: Wakati mwanaye staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, mama yake mzazi, Sanura Kassim ‘Sandra’, mzazi mwenzake, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ na mwanaye Tiffah wakiteketeza kiasi cha fedha kinachokadiriwa kufikia  shilingi Mil.100 barani Ulaya walikokwenda kula bata, baba mzazi wa msanii huyo, Abdul Juma anadaiwa kushinda njaa kutokana na ugumu wa maisha, twende na Risasi Jumamosi. Baba mzazi wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Mzee Abdul Juma. Diamond na familia yake hiyo sambamba na madansa wake, waliondoka nchini mwishoni mwa wiki iliyopita kwenda Frankfurt, Ujerumani ambapo pamoja na kufanya ziara ya kimuziki katika nchi tofauti balani Ulaya, staa huyo aliitumia ziara hiyo kuponda raha. Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, mzazi mwenzake, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ pamoja na mtoto wao Tiffah wakila ‘bata’ Ulaya. TUJIUNGE NA CHANZO Chanzo makini kililiambia gazeti h

Majambazi Yaua Wawili Mwanza, Saba Wajeruhiwa

Image
Kamanda wa Polisi Mkoani Mwanza, SACP Justus Mamugisha, akitoa taarifa kwa wanahabari. Wanahabari wakifuatilia habari ya Kamanda Kamugisha. Mwanza WATU wawili wameuawa Jijini Mwanza kwa kupigwa risasi na Majambazi, huku Wengine saba wakijeruhiwa katika tukio la uvamizi wa duka lililokuwa likitoa huduma mbalimbali za kifedha. Kamanda wa Polisi Mkoani Mwanza, Justus Kamugisha, amesema kuwa tukio hilo lilitokea jana majira ya saa mbili usiku katika eneo la Bugarika Sokoni, baada ya watu watatu wanaosadikika kuwa ni majambazi waliokuwa na bunduki aina ya SMG kuvamia katika duka la mfanyabiashara na mkazi wa eneo hilo aitwae Daniel Marwa (30). Kamanda Kamugisha amewataja waliouawa kuwa ni Julius Wankaba (30) ambae ni dereva bodaboda, pamoja na mfanyabiashara mmoja mwenye duka katika eneo hilo aliefahamika kwa jina la Mama Yuni (35). Amewataka waliojeruhiwa kuwa ni Magesa Mungari (38), Simioni Charles (26) ambao wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa Bugando huku

Mwanasheria Mkuu Zanzibar Aapishwa Rasmi

Image
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein akimuapisha Bwana Said Hassan Said kuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, hafla iliyofanyika ukumbi wa mikutano Ikulu Mjini Unguja. . RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein leo amemuapisha Bwana Said Hassan Said, kuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar. Wageni waliohudhuria kwenye hafla hiyo ya kuapishwa kwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar. Rais wa Zanzibar na Mwenyeikiti wa Baraza la Mapinduzi alimteua Bw. Said Hassan jana kushika wadhifa huo kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya Kifungu cha 55 (1) cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984. Hafla ya kumuapisha Mwanasheria Mkuu huyo ilifanyika Ikulu Mjini Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Miongoni mwao ni Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe. Omar Othman Makungu, Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee, Mkuu wa Mkoa wa Mjini Ma

Dai Risiti Popote Utakapotoa Fedha Kupata Huduma

Image
TUPO hapa kwa ajili ya kuiendeleza nchi yetu, kama tusipoiendeleza Tanzania, basi jua hakuna mtu atakayeweza kufanya hivyo, kama leo hautolia kwa ajili ya Tanzania, usifikiri kuna mtu atakuja kulia kutoka nchi nyingine. Tunahitaji Tanzania ibadilike, hakuna atakayeweza kuibadilisha Tanzania isipokuwa Mtanzania mwenyewe. TRA ikishirikiana na Tanzania Youth Patriot (TYP) inakusisitiza ndugu Mtanzania kwamba popote utakaponunua kitu au kupata huduma fulani kwa gharama yoyote ile dai risiti.   Hii itaiwezeshesha serikali kupata kodi ambayo moja kwa moja itakwenda kufanya kazi katika jamii yetu. Kupitia hela hiyo, hospitali zitajengwa, watoto wataendelea kupata elimu bure, dawa zitaongezwa hospitalini na vitu vingine vyote kwa manufaa ya Watanzania wote. Ndugu zangu, kumbuka kwamba mtu pekee anayeweza kuibadilisha Tanzania ni Mtanzania pekee na si mtu mwingine. Bado tunahitaji vijana wengi wa kuibadilisha Tanzania yetu! Je upo tayari kuungana nasi?

Nay, Dayna Aibu Yao!

Image
  Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ akiwa katika pozi la nusu utupu na msanii wa Bongo Fleva, Aisha Nyange ‘Dayna’. NA BONIPHACE NGUMIJE,  Risasi Jumamosi DAR ES SALAAM: Hii ni aibu yao! Picha zinazomuonesha staa wa Hip Hop anayetamba na ngoma ya Shika Adabu Yako, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ akiwa katika pozi la nusu utupu na msanii wa Bongo Fleva, Aisha Nyange ‘Dayna’ zimevuja pasipo wenyewe kujua.   Katika baadhi ya picha hizo, Nay anaonekana akiwa amemkumbatia Dyna huku wakiwa hawana nguo za juu, yaani Nay hana vesti wala tisheti na hata Dyna akiwa hana nguo yoyote ya kumstiri juu. Baada ya kuzidaka picha hizo gazeti hili lilivuta waya na kuwatafuta wahusika ambapo baada ya kumpata Nay na kumdadisi kama anabanjuka kimalovee na mwanadada huyo alikuwa na haya ya kusema;   “Dah, hapana bwana, hizo picha hatukupanga zitoke. Kuna ambazo zilipitiliza si unajua wakati wa kupiga studio zipo ambazo huwa hamzitumii sasa sijui nani alizivujisha hizo mbaya

Mchezaji wa Sunderland, Adam Johnson ahukumiwa miaka sita jela baada ya kujihusisha kimapenzi na binti wa miaka 15

Image
Mchezaji wa mpira wa miguu, Adam Johnson amehukumiwa kifungo cha miaka sita jela baada ya kukutwa na hatia ya kufanya mapenzi na binti wa miaka 15. Jaji alimwambia kuwa hajaonesha majuto yoyote kutokana na kitendo chake na ni makosa yake mwenyewe “This will be your first prison sentence, this is all entirely your fault.” Mchezaji huyo ambaye alikuwa analipwa pound 60,000 kwa wiki ataanza kutumikia kifungo chake leo baada ya kuhukumiwa na jaji Jonathan Rose.

Ray C absence on social media continues to spark rumours that she is back to abusing drugs.

Image
Ray C absence on social media continues to spark rumours that she is back to abusing drugs. This is however not new as a certain tabloid reported she was spotted at her usual crack house. But the singer came forth to brush off the rumours and threatened to sue those spreading the rumours. Well, her own fans have stepped in to urge to quit drugs for good. From the few comments on her gram, most fans think she is indeed back to her usual ways. Apparently the Methadol (mainly used in the treatment of narcotic dependence) is slowly pulling her back to popping pills. So far nothing has changed about her and the career she holds on to is slowly dying. Anyway, she has however not said not anything about the comments.