Posts

Breaking News: Moto Waunguza Shule ya Wasichana Korogwe

Image
Shule ya Sekondari ya Wasichana Korogwe  iliyoko wilayani Korogwe Mkoa wa Tanga, inaungua moto usiku huu, huku chanzo cha ajali ya moto huo kikiwa hakijajulikana. Inadaiwa watu kadhaa wamejeruhiwa kutokana na moto huo. Hakuna vifo vilivyoripotiwa ama kuthibitishwa hadi sasa. Tunaendelea kufuatilia kwa kina, taarifa zaidi tutakuletea baadaye.

Breaking News: Watano Wafariki Basi la New Force Kugongana na Hiace

Image
WATU watano wamefariki dunia leo asubuhi baada ya basi la New Force lilikokuwa linatokea Msamvu kwenda Mikese kugongana na gari dogo la abiria (Hiace) lililokuwa linatokea Msamvu, mkoani Mogororo. Pia watu kadhaa ambao idadi yao bado haijajulikana, wamejeruhiwa. Mashuhuda wa ajali hiyo wanasema chanzo ni dereva wa gari hilo la Hiace kutaka kulipita gari la mchanga lililokuwa mbele ambapo lilijikuta likigongana uso kwa uso na basi hilo.