Beny Kinyaiya Afungukia Ishu Ya Ushoga, Awaanika Wanay
Mtangazaji maarufu wa kituo cha runinga, Beny Kinyaiya. MAKALA: HASHIM AZIZ Wengi wanamfahamu kupitia shoo zake za runinga zilizompa umaarufu mkubwa, zikiwemo Afro Beats alipokuwa East Africa TV, Ben & Mai Live alipokuwa TBC, Mama Land alipokuwa Clouds TV na sasa Kinyaiya’s Corner akiwa Channel Ten, namzungumzia Beny Kinyaiya ambaye leo tunaye kwenye Mtu Kati. Mwandishi wetu alifanya mahojiano na Kinyaiya ambapo alifunguka mambo mbalimbali, ikiwemo tuhuma zinazomuandama kwa kipindi kirefu, za madai ya kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja (ushoga), uhusiano wake wa kimapenzi na wanawake mbalimbali, pamoja na ishu zinazomuweka mjini. Mahojiano yalikuwa kama ifuatavyo: Mtu Kati: Mambo vipi Beny. Kinyaiya: Poa tu! Mtu Kati: Ukiachilia mbali utangazaji wa runinga, una ishu gani nyingine zinazokuweka mjini? Kinyaiya: Mimi ni mfanyabiashara, mjasiriamali na msanii. Nina biashara zangu kibao mjini lakini siwezi kuzitaja hadharani, kama hiyo haitoshi, namiliki ba