MREMBO ANASWA LIVE AKIFANYA BIASHARA YA NGONO NJE YA OFISI YA SERIKALI.
Mrembo aliyekuwa akijihusisha na biashara haramu ya ngono nje ya ofisi za serikali akikurupuka mara baada ya kunaswa mtegoni. Njaa mbaya! Kama ulikuwa unadhani ile Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers imenywea, basi umenoa! Safari hii imenasa tukio la mrembo akijihusisha na biashara haramu ya ngono nje ya ofisi za serikali, Ijumaa Wikienda lina kitu laivu. Tukio hilo lisilo la kimaadili lilijiri usiku wa manane wikiendi iliyopita kwenye ofisi ya Mtendaji wa Kata ya Kijitonyama, Dar. Baada ya kupokea kero kwa wakazi wazalendo wa eneo hilo kuwa ofisi yao inanajisiwa, OFM ilifanya uchunguzi wake wa kina na ilipojiridhisha ndipo ikaweka mtego. Kabla ya tukio ilisemekana kuwa pamoja na ngono kufanyika waziwazi na machangudoa waliopo maeneo mbalimbali ya Sinza na Kijitonyama, Dar, siku hizi wadada hao wafikia hatua mbaya zaidi kwa kufanyia maeneo yenye hadhi na sifa maalum kama viwanja vya shule za msingi, nje ya ofisi za watu, karibu na misikiti na makanisani. Timu ya OFM k