Posts

Kayumba Amuumbua Mkubwa Fela

Image
Akiongea kwenye Planet Bongo ya East Afrika Radio, Kayumba amesema pesa bado ipo ingawa imeshapungua, tofauti na alivyosema Mkubwa Fela, na kwamba hata ujenzi wa nyumba bado unaendelea. Kayumba “Hela ipo, ingawa sio tena milioni 50 , itakuwa uwongo nikisema bado ipo milioni 50, lakini zipo siwezi kusema imebakia ngapi, si unaona napendeza nini, nyumba ipo kama nyumba zingine, kawaida siwezi kuzungumzia labda vyumba vingapi, ili mradi nitaweka ubavu wangu nitashukuru Mungu”, alisema Kayumba. Hivi Karibuni kulikuwa na tetesi ambazo zilipigiwa mstari na bosi wa msanii huyo Mkubwa Fela, kwamba pesa alizoshinda msanii huyo zilishaisha kitambo, na nyumba yake ya kuishi ikiwa bado haijakamilika. eatv.tv

Zifahamu Faida/Hasara za kurudiana na Mpenzi wako wa zamani

Image
Kuna faida ya wapenzi kuachana na kurudiana? Vipi kuhusu hasara zake? Hiyo ndiyo mada yetu ya leo kama inavyojieleza. Bila shaka unawajua watu ambao walikuwa wakiishi pamoja kimapenzi, iwe ni ndoa, uchumba au uhusiano wa kawaida ambao wamewahi kutengana na baadaye wakarudiana, iwe ni mara moja au zaidi. Yawezekana hata wewe ukawa miongoni mwa watu wa aina hiyo, kwamba uliwahi kutengana na mtu umpendaye lakini baadaye ukajikuta unarudiana naye na kuanzisha upya uhusiano. Je, kuna faida na madhara gani kwa wapenzi kuachana kisha kuja kurudiana tena na kuanzisha upya uhusiano wa kimapenzi? Ukiwaona watu wanaoishi kwenye aina hii ya uhusiano wa kimapenzi unawachukuliaje? NI JAMBO LA KAWAIDA KATIKA MAPENZI Yawezekana aina hii ya uhusiano wa kuachana na kila mmoja akaendelea na maisha yake kisha baada ya muda mkarudiana tena, likaonekana jambo la ajabu au geni katika mila na desturi za Kiafrika lakini kwa taarifa yako, hili ni jambo la kawaida kabisa katika uhusiano wa kimapenz

MATUKIO MBALIMBALI KATIKA ZIARA YA RAIS WA RWANDA PAUL KAGAME

Image
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wageni mbalimbali wa ndani na nje ya nchi wakati wa dhifa ya Kitaifa aliyomwandalia Rais wa Rwanda Paul Kagame Ikulu jijini Dar es Salaam.  Rais wa Rwanda Paul Kagame akizungumza na wageni mbalimbali katika dhifa ya kitaifa aliyoandaliwa na mwenyeji wake Rais Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam.  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Waziri Mkuu mstaafu Salim Ahmed Salim Ikulu jijini Dar es Salaam mara baada ya kumalizika kwa dhifa ya kitaifa aliyomwandalia Rais wa Rwanda Paul Kagame.  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Rais Mstaafu wa awamu ya pili Alhaji Ali Hassan Mwinyi Ikulu jijini Dar es Salaam mara baada ya kumalizika kwa dhifa ya kitaifa aliyomwandalia Rais wa Rwanda Paul Kagame.  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akijadiliana jambo na Ma

Msanii wa Diamond Atuhumiwa Kumbaka Mrembo Jack Wolper....Jack Wolper Afunguka Makubwa

Image
Habari iliyoandikwa kwenye gazeti la Sani la leo jumamosi limemsononesha mrembo Jack Wolper kwa tuhuma za uongo kuwa amebakwa na Msanii wa Diamond... Mwenye Kayaandika haya kwenye ukurasa wake wa Instagram: @wolperstylish - I am so sad kwakweli Hii sio kuniabisha mimi tu, ni kuaibisha na wanawake wenzangu, sijui kwanini magazeti ya kibongo yanatumia Nguvu nyingi kushusha hadhi ya wasanii wa kike haswa.. Nyie SANI no wonder mmepotea katika soko.. Hivi mlivyokua mnachapa mmefkiria kuna wadogo zangu wanasoma?? Au mama angu na baba angu! Naandika kwa uchungu kwakua najua ni limtu limekosa kazi ya kutumia kipaji chake na karama yake vyema linaishia kutumia kwa kuniharibia maisha yangu... Tena front page? Tunafany mangapi mazuri hatuingii page ya kwanza hata siku moja,?! Kesho kutwa nafungua biashara mtaona kama wataandika kitu Ila kwenye ujinga wa kutunga ndo wakwaza Mnaniuzi na nawahakikishia kama Mungu aishivyo mtaona kwa wanenu pia Si mmeamua kuniandika mimi hivi!??

Tamko la RC Makonda kuhusu mashoga waliopo jijini Dar es Salaam

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda ametangaza vita na makaka poa (mashoga) na madada poa (makahaba) walioko jijini Dar es Salaam kuwa utaendeshwa msako mkali wa kuwaondoa. Mkuu wa Mkoa huyo aliyasema hayo kufuatia hali ya vitendo hivyo visiyokubalika na jamii kuzidi kushamiri na kuwa kuna hatari kubwa ya watoto wadogo kuiga vitendo hivyo vinavyoleta picha mbaya kwani ni kinyume na maadili ya mtanzania. Aidha alisema hawezi kuifumbia macho hali hii kwani inamomonyoa maadali ya jamii na kuwa yuko tayari kulivalia njuga suala hili ili kuhakikisha anawamaliza wote mkoani Sakati hili la ushoga na ukahaba limeibuka siku za hivi karibuni baada ya kituo cha televisheni cha Clouds Tv kumhoji shoga mmoja ambapo jamii ilipinga kitendo hicho na kuona kama walikuwa wakiuhalalisha ushoga na kuaminisha jamii kuwa ni kitu kizuri.

Nilivyofanya Bonge la Sherehe Baada ya Mke Wangu Kufukuzwa Kazi

Image
Huyu mke nilimuoa akiwa hana kitu, kwa bahati alitafutiwa kazi na ndugu yake kwenye kampuni moja ya simu akawa analipwa kama milioni 3 kwa mwezi fasheni na yeye yeye na fasheni vipodozi kila aina,handbag na nywele za laki mbili ndio mshahara wake ukawa unaishia huko mimi mshahara wangu hauzidi laki sita,nilifanyishwa vituko vyote ndani ya nyumba ,manyanyaso yote ,hapiki hafui,hafanyi chochote ndoa ikawa inaelekea kuvunjika. Nikaenda mahakamani kuprocess talaka wakasema mpaka nianzie baraza la usuluhishi la kata au kanisani,nikaamua kwenda kanisa tulilofungia ndoa tukaitwa kwa Baba Paroko for hearing sijui mediation sijui arbitration sijui mie nikatinga kwa bajaj ya kukodi nimepaukaaa yeye akaja na RAV4 . Baba Paroko alivyotusikiliza akaaniita pembeni akasema kijana hapa nadhani hata tukiomba na kukariri mistari yote ya biblia plus mapambio yote ndoa yako haitarudi kama mwanzo pambana utafute hela ,huyu ni mchaga katumwa pesa mjini Nilisali sana nikasugua goti n

Mbunge Chadema Avuliwa Ubunge

Image
Aliyekuwa Mbunge wa Longido, Mhe. ONESMO NANGOLE. Kesi iliyokuwa inaunguruma kuanzia tarehe 29.02.2016 katika Mahakama Kuu jijini Arusha imetolewa hukumu leo hii. Katika shauri hilo aliyekuwa mgombea Ubunge wa CCM, Jimbo la Longido, Dk. KIRUSWA alifikisha mahakamani shauri hilo la kupinga matokeo ya ushindi dhidi ya Mbunge wa Longido, Mhe. ONESMO NANGOLE. Akisoma hukumu hiyo, Jaji MWAGESI alisema kwamba mlalamikaji ndugu Kiruswa aliwakilishwa na Wakili Dk. Masumbuko Lamwai na Wakili Haraka. Katika shauri hilo, dai la msingi la mlalamikaji bwana Kiruswa lilikuwa ni; 1.Kutumika kwa lugha ya matusi na kashfa wakati wa kampeni kutoka kwa Mhe. Onesmo Nangole 2.Kuwepo kwa wapiga kura kutoka nchi jirani ya Kenya walioletwa na Mhe. Nangole 3.Kutumika kwa magari ya Chadema kwenye kusindikiza na kubebea masanduku ya kupigia kura 4.Mkurugenzi wa Uchaguzi kutangaza matokeo baada ya mgombea wa CCM kutolewa nje. 5.Kutokea kwa vurugu ndani ya chumba cha kuhesabu matok

MKUFUNZI WA MASWALA YA BIASHARA NA MASOKO REHEMA KASULE AWAPA ELIMU MANJANO DREAM MAKERS

Image
Mkufunzi wa maswala ya biashara Mama Rehema Kasule kutoka nchini Uganda akiwapa elimu wanafunzi wa Manjano Foundation jinsi ya kukabiliana na changamoto zinazowakabili kwenye majukumu yao ya kila siku ikiwemo kutengeneza uhusiano na watu waliofanikiwa kwa kuwa itasaidia kujifunza mengi. Pia namna ya kujiamini kuwaza mafanikio zaidi kuwa lazima wafanikiwe na kuachana kabisa na mawazo ya kushindwa akiwa sambamba na Afisa mtendaji mkuu wa Shear illusions, Mama Shekha Nasser.  Akieleza zaidi Mama Kasule amewataka Washiriki wa Manjano Dream Makers kama wanataka kufanikiwa kazi zao za upambaji na biashara zao ni lazima wafanye kwa moyo mmoja kutoka ndani ya nafsi pia kuachana na fikra za kukata tamaa na maneno ya watu ya kuwakatisha tamaa. Kwa upande afisa mtendaji mkuu wa Shear illusions na Mkurugenzi wa Manjano Foundation mama Shekha Nasser amewataka washiriki hao kuongeza juhudi pia kuyatekeleza kwa vitendo yale yote waliofundishwa katika mafunzo hayo. Mama Rehmah Kasule al

TP MAZEMBE YAIKONG’OLI YANGA KAMOJA UWANJA WA TAIFA

Image
Mshambuliaji wa timu ya Yanga,Obrey Chirwa akiichambua ngome ya timu ya TP Mazembe, katika mtanange uliopigwa jioni hii kwenye dimba la Taifa (Uwanja wa Taifa) Jijini Dar es salaam, ikiwa ni Mchezo wa Kombe la Shirikisho Barani Afrika. Hadi kupanga cha mwisho kinalia, Yanga wamelala kwa bao 1-0.(Picha na michuziblog) Mashabiki wakiwa wamefurikwa kwenye uwanja wa Taifa hata hivyo mwishowe wakaondoka vichwa chini baada ya timu yao kupoteza mchezo huo mbele ya mahasimu wao TP Mazembe

SEKTA YA MAWASILIANO KUPATA MWEKEZAJI ZAIDI

Image
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayesimamia sekta ya Mawasiliano Prof. Faustin Kamuzora akizungumza na ujumbe kutoka Kampuni ya Oracle Afrika (hawapo pichani) walipomtembelea ofisini kwake kwa nia ya ushirikiano katika kulinda miundombinu na mifumo ya TEHAMA. Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayesimamia sekta ya Mawasiliano Prof. Faustin Kamuzora (kulia) akimsikiliza Mkurugenzi mtendaji wa Kampuni ya Oracle Afrika Bw. Cherian Varghese (katikati) akielezea nia ya Kampuni yao katika ushirikiano wa kulinda miundombinu na mifumo ya TEHAMA hapa nchini. Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayesimamia sekta ya Mawasiliano Dkt. Mhandisi Maria Sasabo (wa kwanza kushoto) akizungumza na ujumbe kutoka Kampuni ya Oracle Afrika walipotembelea sekta ya Mawasiliano na kueleza nia yao ya ushirikiano katika kulinda miundombinu na mifumo ya TEHAMA. ……………………………………………………………………………. Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uc

Black Coffee Ashinda Tuzo ya BET ya Best International Act Africa

Image
Black Coffee baada ya kupokea tuzo yake. Black Coffee akiwa na mkewe Enhle Mbali Mlotshwa. Black Coffee na mkewe wakiwa kwenye pozi na baadhi ya mastaa kutoka Afrika akiwemo Akon na AKA.   Black Coffee katika pozi. Black Coffee amekuwa mwanamuziki wa kwanza kutoka Afrika Kusini kutwaa tuzo ya BET katika kipengere cha ‘Best International Act Africa 2016’ na kuwapiku mastaa wengine walioteuliwa kuwania tuzo hiyo akiwemo Diamond Platnumz. Black Coffee mwenye umri wa miaka 40, ametwaa tuzo hiyo huko Los Angeles nchini Marekani akiwabwaga wasanii wenzake ambao ni AKA‚ Cassper Nyovest‚ Diamond Platnumz‚ MzVee‚ Serge Beynaud‚ Wizkid na Yemi Alade waliokuwa wanawania tuzo hiyo.

Rais Magufuli Afanya Mabadiliko ya Ma RC na Ma DC

Image
Rais Dk. John Pombe Magufuli. Rais Dk. Magufuli amefanya mabadiliko madogo ya wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya, atengua uteuzi wa Mkuu wa Mkoa wa Mara, Magesa Mulongo na kuteua Ma DC 139. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 26 Juni, 2016 amefanya mabadiliko madogo katika safu ya wakuu wa mikoa na amewateua wakuu wa wilaya 139. Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi amesema katika mabadiliko hayo Rais Magufuli amemteua aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Bi. Zainab R. Telack kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga. Bi. Zainab R. Telack anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Anna Kilango Malecela ambaye uteuzi wake ulitenguliwa. Rais Magufuli pia amemteua Dkt. Binilith Satano Mahenge kuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma. Dkt. Binilith Satano Mahenge anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Said Thabit Mwambungu ambaye amehamishiwa Ofisi ya Waziri Mkuu Dar es salaam am

Meli ya Mizigo Yazama Unguja

Image
Zoezi la uokoaji likiendelea eneo ilipozama meli ya MV Happy. Meli ya mizigo iitwayo MV Happy iliyokuwa ikitokea jijini Dar es Salaam kwenda Zanzibar imezama leo asubuhi kwenye Bahari ya Hindi eneo la Chumbe, Unguja. Kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo ni kwamba meli hiyo ilianza kuzama majira ya saa 10 alfajiri na kufikia saa moja asubuhi ilikuwa imezama kabisa ndani ya maji. Wananchi wakishuhudia zoezi la uokoaji. Mpaka sasa hakuna vifo vilivyoripotiwa bali mizigo iliyokuwemo kwenye meli hiyo ndiyo iliyozama. Taarifa zaidi zitaendelea kuwajia kupitia tovuti hii.

Tanzia: Aliyekuwa Mbunge wa Biharamulo Magharibi (2010-2015) Afariki

Image
Dk. Antony Gervase Mbassa enzi za uhai wake. Aliyekuwa Mbunge wa Biharamulo Magharibi (2010-2015) kupitia CHADEMA, Dk. Antony Gervase Mbassa amefariki dunia ghafla usiku wa kuamkia leo nyumbani kwake.

RAIS DKT MAGUFULI AZINDUA MPANGO WA KITAIFA WA KITUO CHA MAWASILIANO CHA JESHI LA POLISI (CALL CENTRE)

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akikagua kituo cha mawasiliano ya polisi (Call centre) katika kituo cha Kati jijini Dar es salaam wakati wa uzinduzi wa Kitaifa wa Kituo cha Mawasiliano cha Jeshi la Polisi. .Pamoja naye ni Waziri wa mambo ya Ndani Mhe Mwigulu Nchemba, Katibu Mkuu Wizara ya mambo ya Ndani Meja Jenerali Projest  Rwegasira, IGP Ernest manu, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul Makonda na viongozi wengine  wa sekta ya umma na binfasi. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli  akikagua kituo cha mawasiliano ya polisi (Call centre) katika kituo cha Kati jijini Dar es salaam wakati wa uzinduzi wa Kitaifa wa Kituo cha Mawasiliano cha Jeshi la Polisi. .Pamoja naye ni Waziri wa mambo ya Ndani Mhe Mwigulu Nchemba, Katibu Mkuu Wizara ya mambo ya Ndani Meja Jenerali Projest  Rwegasira, IGP Ernest manu, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul Makonda na viongozi wengine  wa sekta ya umma na binfasi. Rais