Posts

MAKUBWA YAFUCHUKA HOUSIGELI ALIYETESWA KWA MIAKA 3 KWA KUCHOMWA NA PASI NA BOSI WAKE

Image
NYUMAya pazia! Yule msichana Yusta Lucas (20) mwenyeji wa Mkoa wa Tabora ambaye alifika jijini Dar kufanya kazi ya u-hausigeli na kufanyiwa ukatili wa kutisha na bosi wake kisha habari zake kuandikwa, ametoa siri nzito, Uwazi limemegewa.Yusta Lucas akionyesha majeraha ya meno aliyong'atwa na bosi yake . Akizungumza kwa uchungu na gazeti hili akiwa wodini kwenye Hospitali ya Mkoa wa Kitabibu Kino ndoni, Mwananyamala jijini Dar, Yusta ambaye amefanya kazi kwa tajiri yake huyo kwa miaka mitatu alisema: “Kwanza nataka watu wajue kuwa mwajiri wangu ni binamu yangu, alinileta hapa Dar kwa ajili  ya kumsaidia kazi za ndani pamoja na kumlelea mwanaye. “Kipigo hasa kilianza mwanzoni mwa mwaka huu ikiwa ni pamoja na kuning’ata kwa meno mwili mzima, ndiyo maana mwili wangu wote unaonekana una mabakamabaka. “Mateso yangu majirani walikuwa wakiyajua kutokana na kilio changu lakini walikuwa wanashindwa kunisaidia kwa sababu ya ushirikiano mdogo. “Kwanza nashangaa

KIJANA ALIYEJIPIGA RISASI ARUSHA, MAMBO YA AJABU YATOKEA KABLA NA WAKATI AKIJIUA

Image
Mapema leo nilikupatia story kuhusiana na kijana matata Richard Mollel pesa chafu ambaye amejipiga risasi Arusha, sasa nimepata muendelezo wa matukio ya ajabu yaliyomtokea kijana huyo kabla ya kifo chake mpaka alipojiua. Yaani ndio nimetokea hapo kwake kwani ni ajabu kabisa.Alikuwa na girl friend wake kwenye gari kufika eneo la Mount Meru akagonga Hiace kwa nyuma gari ikabonyea lakini yeye na mpenziwe wakatoka wazima bint anadai baada ya dakika km 2 akahisi kizunguzungu akaanguka chini kuja kushtuka anaona watu wengi na kijana naye kutoka hapo akatimka mpaka k aribu na nyumbani kwake ndio kujipiga risasi na kufa.Sasa bint anaulizwa mlikuwa na ugomvi anasema wala yeye mwenyewe anashangaa kilichomkuta keshatoka mzima kwenye ajali kukimbia na kwenda kujiua.Ni kijana wa 86 yaani mdogo kabisa na ndio pesa imekubali na baba yake ni mgonjwa yuko hoi muda huo yenyewe alikuwa amepigiwa cmu na dada zake aende kumuogesha maana ni mtt pekee wa kiume na ndio alikuwa

AIBU YA MWAKA: MSANII CHID BENZ AVUTA BANGI UKUMBINI, ATISHIA KUMPIGA DJ NA ATOROKA BILA KULIPIA CHUMBA CHA GUEST

Image
Hapo Chidi Benz akiwa kashikiwa bangi na Shabiki wake na kutoa kibiriti cha gesina kuiwasha kama unavyoona hapo Chini benz Jana Jumapili wakati anafanya show New maisha Club Dodoma alifanya kitendo ambacho baadhi ya mashabiki walimwona kweli jamaa sasa ameshaanza kuwa chizi. Wakati akiwa anafanya Show baada ya mzuka kumpanda Chid alichafua hali ya hewa baada ya kuzama mfukoni na kutoka Bonge la kipisi cha Bangi kilichoshiba na kukiwasha pale pale jukwaani bila hata Uwoga... Hapo ndipo Baunsa wa Maisha kabla akambadilikia kama Mbogo na kumpora hiyo bangi ili asiendelee kuivuta. Kitendo hicho cha kuvuta bangi Club kimeshushia heshima Msanii huyo ambaye ni kioo cha Jamii. Siku za Hivi karibuni Msanii huyo alifanya ndivyosivyo kwenye club moja Mjini Lindi pale alipotishia kumpiga shabiki wake pamoja na Dj. si Hivyo tu aliweza kutoroka Bila kulipa Malipo ya chumba alichofikia kwenye Lodge moja Mjini hapo na Kukimbia Alfajiri kukwepa kulipia Chumba Hicho. H

MZEE SMALL AZIKWA, AACHA LAANA KWA NINI KAACHA LAANA NA KAWAACHIA AKINA NANI? SOMA HAPA

Image
Ustadhi akimuombea marehemu dua ya mwisho baada ya kuuhifadhi mwili wake kaburini. Stori: MWANDISHI WETU HATIMAYE  aliyekuwa nguli wa sanaa za maigizo Bongo, Said Ngamba ‘Mzee Small’ amezikwa jana katika Makaburi ya Tabata-Segerea jijini Dar es Salaam huku akiacha laana kwa tasnia ya maigizo. Mzee Small alifariki dunia usiku wa kuamkia Jumapili kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili  (MNH) ambako alilazwa akisumbuliwa na maradhi ya kiharusi yaliyomuanza miaka takriban miwili iliyopita. Mwili wa Mzee Small ukiwa kaburini. Wakati wa kuugua kwake, marehemu aliwahi kulalamikia kitendo cha sehemu kubwa wa wasanii wa Bongo Movies kumtenga kiasi cha kuwa ombaomba hali iliyomfanya awe akisema: “Mungu yupo, iko siku.” “Mzee Small amezikwa sasa, lakini kichwani lile neno lake kwamba Mungu yupo kwa sababu tulikuwa hatumsaidii kwa lolote naliogopa sana,” alisema mmoja wa mastaa wa Bongo Muvi ambaye hakupenda jina lake litoke gazetini.   Mdogo wa marehemu mzee Small ak

BOKO HARAM WATEKA WANAWAKE WENGINE 20 NCHINI NIGERIA

Image
Wapiganaji wanaoshukiwa kuwa wanachama wa Boko Haram wamewateka nyara wanawake 20 kutoka jamii inayohamahama Kaskazini Mashariki mwa Nigeria.   Wanawake hao walichukuliwa katika Makazi ya Gakini Fulani karibu na mji wa Chibok ambako zaidi ya wasichana wanafunzi 200 walitekwa nyara Aprili, mwaka huu. Walioshuhudia tukio hilo walisema kuwa wapiganaji hao waliokuwa wamejihami kwa bunduki waliwalazimisha wanawake hao kuingia katika magari yao kabla ya kutoroka nao katika Jimbo la Borno.   Mlinzi mmoja wa kijiji alisema kuwa washambulizi hao pia waliwateka nyara wanaume watatu waliojaribu kuwazuia wasiondoke na wanawake hao. Hadi sasa jeshi halijasema lo lote kuhusiana na tukio hilo.   Katika  hatua  nyingine,  jeshi la Nigeria limesema kuwa limewaua wapiganaji 50 katika kampeni yake dhidi ya magaidi mwishoni mwa wiki katika majimbo ya Borno na Aladawa.   Mfululizo wa mashambulizi Kaskazini Mashariki mwa taifa hilo umeimarisha ukosoaji wa vyo

KIJANA ALIKUFA AIBUKA AWA MSUKULE POLISI WAPIGWA BUTWAA

Image
Kijana   Kenedy Onyango Augustine aliyedaiwa kupotea kimiujiza amerudi nyumbani akiwa hai baada ya kudaiwa kuwa alikuwa amechukuliwa msukule. KIJANA  Kenedy Onyango Augustine (22),  mkazi wa Kitongoji cha Nyambogo Shuleni, Kata ya Kitembe wilayani Rorya mkoani Mara aliyepotea kimiujiza amerudi nyumbani akiwa hai baada ya kudaiwa kuwa alikuwa amechukuliwa msukule. Baba mzazi wa kijana huyo, Augustine Oyoo alisema kuwa kijana wake alipotea katika mazingira ya kutatanisha wakati alipokuwa anakwenda kulala nyumbani kwa baba yake mdogo, Raubeni Oyoo kijijini hapo.‘’Kijana wangu aliondoka saa tatu usiku Juni 3, mwaka huu baada ya kula chakula cha usiku na kwenda kulala kwa baba yake mdogo alikokuwa akilala. “Ajabu hakufika, asubuhi tulianza kumsaka bila mafanikio ndipo tulipochukua hatua za kumtafuta kwa majirani lakini jitihada hizo hazikuzaa matunda ambapo walituambia kuwa hawakumuona,’’ alisema Augustine.   Aliongeza kuwa, baada ya kushindwa kumpata walitoa taari

SOMA JINSI WANAWAKE WANAVYO-SHAMBULIWA NA U.T.I

Image
U.T.I  kirefu chake ni Urinary Tract Infection ni maambukizi ya bakteria mbalimbali wanaoshambulia  mfumo wa mkojo, yaani kwenye figo (kidney), kibofu cha mkojo na mifereji inayotoa mkojo (urethra) Mifereji inayotoa mkojo kwenye figo (ureter) na mfereji unaotoa mkojo nje, mara nyingi bakteria hushambulia sehemu za chini za mfumo wa mkojo yaani urinary bladder na kitaalamu kuitwa bladder infection. Bakteria hao baada ya kumuingia binadamu hupona mara moja  pindi mgonjwa anapoanza dozi lakini kama wadudu hawa hawatatibiwa vizuri wanaweza kupanda na kushambulia figo na mshipa unaounga sehemu hiyo uitwao renal pelvis na kuleta madhara makubwa, hivyo kusababisha ugonjwa wa figo. Kuna wadudu wanaotoka kwenye utumbo mkubwa wa binadamu ambao kila binadamu anaishi nao, hawa husaidia kulinda mwili na kitaalamu hujulikana kama  normal flora na huwa ni askari wa mwili. Vijidudu hivyo hushuka hadi kwenye mlango wa  haja kubwa na kuenea mpaka sehemu za siri. Kama watai

ANGALIA PICHA DAKTARI APIGANA NA MGONJWA WODINI MORO

Image
Mwili wa marehemu Yasin Jailan (15) aliyekata roho ndani ya wodi namba tisa katika Hospitali ya Rufaa ya Morogoro huku dokta akizichapa kavukavu. Akiwa mitaani akisaka matukio, mwanahabari wetu alivutiwa waya na chanzo chetu kisha akatonywa kuwa kuna bonge la timbwili kwenye wodi namba tisa katika Hospitali ya Rufaa ya  Timbwili!  Katika hali ya kusikitisha mgonjwa Yasin Jailan (15) aliyekuwa wodini anadaiwa kukata roho huku dokta akizichapa kavukavu na wagonjwa, Ijumaa Wikienda limenasa kisa cha ajabu Morogoro ambapo alitii wito na kufika eneo la tukio ndani ya dakika sifuri (huwa Global hatulazi damu kufika eneo la tukio). Alipofika wodini hapo, mwandishi wetu alishuhudia mtoto akikata roho huku baba mwenye mgonjwa aliyetajwa kwa jina la Jailan Mrisho akizichapa na daktari ambaye jina halikupatikana. Baba wa marehemu (kushoto) akilia kwa uchungu. Kwa mujibu wa baba mwenye mgonjwa, alimfikisha mwanaye hospitalini hapo akisumbuliwa na ugonjwa wa malaria uliokuwa umepa

RAY C sasa kuja na taarab, ampa tahadhari Khadija Kopa,mashahuzi…

Image
Msanii wa muziki Rehema Chalamila aka Ray C amefunguka kwa kudai kuwa ujio wake mpya kwenye muziki atakuja pia na nyimbo za taarab, huku akimtaka Khadija Kopa ajiandae.   Akizungumza na Sporah Show hivi karibuni, Ray C amesema kwenye albam yake ambayo inakuja hivi karibuni kunamchanyiko wa nyimbo mbalimbali zikiwemo taarab na zakihindi. “Nimefanya taarab kama mbili na zook, yani nimebadilishika kabisa, kuna kwaito , kuna bongoflave ,uwindi hindi kidogo, taarab nimeimba pia ,kwaiyo Khadija Kopa ajiandae” Alisema Ray C. Pia Ray amedai kuwa aina ya muziki anaokujanao kwa sasa hivi ni ule wa kuonyesha kipaji chake zaidi cha kuimba na siyo kucheza.

LULU, NANDO WA BBA MAMBO HADHARANI

Image
Mambo hadharani! Uhusiano wa staa wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ na mshiriki wa Shindano la Big Brother Africa 2013, Amir Nando umewekwa kweupe. Muigizaji katika tasnia ya Muvi Bongo, Elizabeth Michael 'Lulu'. Kabla ya wawili hao kufunguka, kulikuwa na madai mazito kuwa Lulu na Nando ‘wanachepuka’ mara tu baada ya Nando kutolewa BBA kwa ukosefu wa nidhamu. Kuna habari kuwa Nando ndiye aliyevujisha ishu hiyo, jambo ambalo Lulu hakupendezwa nalo hivyo kumpiga chini. Mshiriki wa Shindano la Big Brother Africa 2013, Amir Nando. Baada ya kunyetishiwa ishu hiyo, gazeti hili lilimtafuta Nando ambaye mwanzoni alifanya kama utani akidai Lulu ni mwanamke anayefaa kuolewa (wife material) lakini alipoulizwa kwa msisitizo, alikana kuwa na uhusiano na mrembo huyo. Nando akifunguka kuhusu uhusiano wake na Lulu. Kushoto ni Sifael Paul. “Lulu ni mkali, niko tayari kumuoa lakini sijamwambia, akikubali freshi nitamuoa. Kwa sasa ni mshikaji wangu tu