Posts

JACKLINE WOLPER YU HOI HOSPITALINI

Image
Msanii wa Filam Tanzania ajulikanae kwa jina la Wolper yuko hoi Hospitalini huku akiomba Dua kwa wapenzi wake wamuombee ili apone haraka. Wolper ameripot taarifa za kuumwa kwake katika akaunti yake ya facebook na kuainisha ugonjwa unaomsumbua ni Maralia na ujumbe huo umesomeka hivi:

MSANII PHARRELL WILLIAMS ALIPOFUNGA NDOA" angalia PICHA

Image
Msanii na Producer Pharrell Williams amefunga ndoa na mpenzi wake wa muda mrefu Helen Lasichanh na kufanya sherehe ndogo kwenye boti huko Miami, Florida. Wapenzi hao wamechagua boti lililoitwa "Never Say Never" na Kwenye sherehe yao wasanii wakubwa kama Busta Ryhmes, Justin Timberlake, Usher na Robin Thicke walikuwepo. Fahamu kuwa Pharrell Williams na Helen Lasichanh wamekuwa na mahusiano kwa muda mrefu sana na zao lake ni mtoto wa kiume mwenye miaka 4 ' Rocket'

Rais Kikwete apendekeza NYERERE DAY iwe siku aliyozaliwa na siyo siku aliyofariki dunia...Una Maoni gani juu ya hili

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete amependekeza kuwa siku ya ‘Nyerere day’ inayoadhimishwa October 14 kila mwaka, iadhimishwe siku aliyozaliwa mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Rais kikwete ameyasema hayo alipokuwa akiwahutubia wananchi mjini Iringa katika maadhimisho ya kilele cha mbio za mwenge wa Uhuru, iliyoambatana na kumbukumbu ya baba wa taifa Mwalimu Julius Nyerere. Amesema anapendekeza siku hiyo iwe siku ya kuzaliwa ili watu washerehekee kwa furaha, wakikumbuka hotuba za Mwalimu. Endapo mapendekezo ya rais yataungwa mkono, Nyerere day itakuwa April 13, kwa kuwa mwalimu alizaliwa siku hiyo mwaka 1922. Una mtazamo gani juu ya pendekezo hili? -timesfm

Mtu mmoja akutwa amejinyonga mjini Morogoro....Jaribu kumwangalia vizuri, huenda ni ndugu yako au rafiki yako

Image
Mtu ambaye jina lake halikufahamika mara moja amekutwa amejinyonga usiku wa kuamkia leo mjini Morogoro.Chanzo cha mtu huyu kujinyonga hakijafahamika. Askari aliyekuwepo eneo la tukio alidai kwamba askari wa doria waliokatiza kwenye eneo hilo majira ya saa 10 usiku walishuhudia mwili wa mtu huyo ukining'inia juu ya mtu na kuanza juhudi za kuutoa mwili huo. Askari akipanda juu ya mti kwaajili ya kuushusha mwili wa marehemu.

Taarifa kuhusu afya ya mwandishi aliyepigwa risasi ( Ufoo Saro ), tarehe ya mazishi ya mpenzi wake aliyempiga risasi na siku ya mazishi ya mama yake mzazi

Image
Hali ya mwandishi wa habari wa Kituo cha Televisheni cha ITV, Ufoo Saro aliyejeruhiwa vibaya baada ya kupigwa risasi mbili juzi huko Kibamba, Dar es Salaam inazidi kuimarika na jana alizungumza na Mwananchi na kusema; “Sijambo, naendelea vizuri.” Ufoo, ambaye amelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, hata hivyo, anazungumza kwa shida kutokana na kukabiliwa na maumivu baada ya kufanyiwa upasuaji juzi. Mwandishi huyo amehamishiwa katika wodi ya upasuaji wa moyo huku kiongozi wa wodi hiyo, ambaye alikataa jina lake kuandikwa, akieleza kuwa walimhamishia huko ili apate muda zaidi wa kupumzika. “Watu wanakuja kwa wingi kumjulia hali, tuliona tumhamishe ili apumzike,” alisema kiongozi huyo. Kabla ya kupelekwa katika wodi hiyo, Ufoo alikuwa katika wodi ya Kibasila na baadaye alihamishiwa katika Chumba cha Wagonjwa Wanaohitaji Uangalizi Maalumu (ICU). Ufoo alipigwa risasi na mzazi mwenzake, Anthery Mushi ambaye alijiua baaday

HIKI NDIO CHANZO kuhusu kupigwa risasi kwa mtangazi wa ITV ( Ufoo Saro ) ambaye mama yake naye AMEFARIKI

Image
Alfajiri ya leo, mtangazaji wa ITV anayejulikana kwa jina la Ufoo Saro amejeruhiwa vibaya kwa kupigwa risasi na mchumba wake ambaye baada ya tukio hilo naye alijipiga risasi na kujiua. Akizungumza na mpekuzi wetu, kamanda Wambura ambaye ni kamanda wa polisi wa mkoa wa kipolisi wa kinondoni amesema tukio hilo limetokea majira ya alfajiri ya leo. Kamanda wambura amedai kuwa mwanaume aliyetenda mauaji hayo ni mchumba wake na alikuwa anafanya kazi katika umoja wa mataifa ( UN ) huko sudani ila bado haijafahamika kitengo alichokuwa akifanyia kazi. Kwa mujibu wa Kamanda Wambura, inasemekana kulikua kuna ugomvi kati ya wawili hao ambapo walishindwa kuelewana na ndipo walipoamua kwenda kwa mama mzazi wa Ufoo Saro(mama mkwe) ili awasuluhishe Baada ya usuluhishi kuanza na kuonekana kuwa tatizo liko kwa mwanaume, mwanaume huyo alimshutumu mama mkwe wake kwamba amekuwa na mazoea ya kumtetea mwanae na ndipo alipotoa bast

MASANJA MKANDAMIZAJI AKIWA ANAKULA BATA NDANI YA JIJI LA OBAMA

Image

TANZANIA, RWANDA NA BURUNDI NA BENKI YA DUNIA ZASAINI MKATABA WA MRADI WA UMEME RUSUMO

Image
  Waziri wa Fedha, Wizara ya Fedha Tanzania Mhe. Dkt. Wiliam Mgimwa katikati akisaini mkataba wa mradi wa umeme wa Rusumo, kulia kwake ni Waziri wa Fedha na Mipango ya Uchumi Burundi Mhe. Tabu Manirakiza, kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Mkakati na Uendeshaji ukanda wa Afrika Bw. Colin Bruce Picha zote na Bi. Ingiahedi Mduma na Bi Eva Valerian – Washington DC   Naibu Katibu Mkuu, Umoja wa nchi za Afrika Mashariki Dkt. Enock Bukuku akimfafanulia jambo Balozi wa Tanzania Marekani na Mexico Mhe. Liberata Mulamula walioko pembeni ni baadhi ya walihudhuria mkutano  wa kusainiwa kwa mkataba wa Rusumo.   Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mgimwa akikabidhiwa mkataba na Mkurugenzi wa Mkakati na Uendeshaji ukanda wa Afrika Bw. Colin Bruce mara baada ya kusaini.   Mawaziri wa  Fedha wa nchi tatu, kutoka  kushoto Waziri wa Fedha na Mipango ya Uchumi wa Burudi Mhe. Tabu Manirakiza, Waziri wa Fedha wa Tanzania Dkt. Wiliam Mgimwa, Mkurugenzi wa Mkakati na Uendeshaji ukanda wa Afrika

Matokeo ya Nani Mtani Jembe kuanza kutangazwa leo

Image
Mwenyekiti wa Simba SC, Aden Rage akiwakabidhi wafanyakazi wa TBL Mbeya wanaoshabikia Simba baada ya kuwashinda wanaoshabikia Yanga katika hafla ya kuzindua kampeni ya Nani Mtani Jembe kwa wafanyakazi wa kiwanda hicho mwishoni mwa wiki jijini Mbeya. Kampeni hiyo inayoendeshwa na Kilimanjaro Premium Lager inawashindanisha mashabiki wa Simba na Yanga. Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Yanga, Mohammed Bhinda akimkabidhi Mariam Martin zawadi baada ya timu yake kushinda mchezo wa kuvuta kamba katika hafla ya kuzindua kampeni ya Nani Mtani Jembe kwa wafanyakazi wa kiwanda hicho mwishoni mwa wiki jijini Mbeya Wafanyakazi akinamama wa TBL Mbeya wakishindana kuvuta kamba katika hafla ya kuzindua kampeni ya Nani Mtani Jembe kwa wafanyakazi wa kiwanda hicho mwishoni mwa wiki jijini Mbeya. Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Yanga, Mohammed Bhinda akimkabidhi Bahati Msokwa zawadi baada ya timu yake kushinda mchezo wa kuvuta kamba katika hafla ya kuzindua kampeni ya Nan

Balozi wa Oman amuaga Rais Kikwete

Image
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Balozi wa Oman nchini anayemaliza muda wake Mhe.Yahya Mousa Al Bakary ikulu jijini Dar es Salaam leo asubuhi. Balozi huyo alikwenda ikulu kumuaga Rais(picha na Freddy Maro)   Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Balozi wa Oman nchini anayemaliza muda wake Mhe.Yahya Mousa Al Bakary ikulu jijini Dar es Salaam leo asubuhi. Balozi huyo alikwenda ikulu kumuaga Rais(picha na Freddy Maro)

"BREAKING NEWZ"MWANDISHI UFO SARO WA ITV AJERUHIWA KWA RISASI

Image
Habari zilizotufikia zinasema Mwandishi wa habari wa ITV Ufo Saro ambaye anaonekana pichani kulia akisalimiana na Rais Jakaya Kikwete katika moja ya kazi zake za kiuandishi amejeruhiwa kwa kupigwa risasi usiku wa kuamkia leo hata hivyo bado taarifa rasmi za chanzo cha tukio hilo hakijafahamika, phars blogspot imeongea kwa njia ya simu na Mkurugenzi wa Radio One Deo Rweyunga ambaye amethibitisha kutokea kwa tukio hilo lakini akasema bado hawajajua chanzo hivi sasa wanakimbizana kujua hali ya majeruhi na vipi atapa huduma za matibabu ambaye amalazwa hospitali ya Muhimbili kwa matibabu zaidi, Tunaendelea kufuatilia na kujua taarifa kamili mara tutakapokuwa tayari tutawajulisha kupitia ukurasa huu. TUTAENDELEA KUKUJUZA ZAIDI

Tanzania receives US $ 113.30 from World Bank for Rusumo Falls Hydropower Plant

Image
The World Bank’s Board of Executive Directors today approved US$340 million for the Regional Rusumo Falls Hydroelectric Project which aims to benefit people in Tanzania, Burundi and Rwanda. This project is the first operation under the World Bank Group Great Lakes Regional Initiative inaugurated by the World Bank Group President Jim Yong Kim during his historic joint visit with UN Secretary General Ban Ki-moon in May 2013. The World Bank financing of a total US$340 million – US$113.30 million to the countries of Tanzania, Burundi and Rwanda comes from the International Development Association (IDA). IDA is one of the largest sources of assistance for the world’s 82 poorest countries, 40 of which are in Africa. Resources from IDA bring positive change for 1.8 billion people living on less than $2 a day. Between 2003 and 2013, IDA provided $256 billion in financing for 3,787 projects in Sub-Saharan Africa. IDA established in 1960, helps the world’s poorest countries by providin g

Hermy B kuungana na Jaji Ian na Juliana katika Tusker Project Fame 6, awashauri watanzania kupiga kura

Image
Baada ya kuwafahamu majaji wawili wa TPF6 ambao ni Ian Mbugua (Kenya) na Juliana Kanyomozi (Uganda), hatimaye jina la jaji wa tatu limefahamika ambapo C.E.O wa BHitz Music, Hermes Bariki a.k.a Hermy B (Tanzania) ndiye atakayeungana na majaji hao wawili. Akiongea na 100.5 Times fm Hermy B amewashauri watanzania kuwasapoti washiriki wanne kutoka Tanzania kwa kuwapigia kura kwa kuwa ushindi hutokana na wingi wa kura anazopigiwa mshiriki na sio anachosema jaji. “Watanzania wasifikirie kwamba Jaji wao ndiye atakayewapatia ushindi washiriki wao, ndio wapige kura sasa, kwa sababu ushindi wa watu wengi unatokana na kura na sio jaji, hata Juliana akimwambia you are the best of the best lakini asipopigiwa kura hawezi kushinda.” Amesema Hermy B. Washiriki watakaoiwakilisha Tanzania katika TPF6 ni Angella Karashani a.k.a Angel, Tanah, Hisia na Dubson. Mshindi wa mwaka huu atapewa shilling Million Mia Moja, na mkataba wa kurekodi nyimbo kwa gharama ya shilingi Mil

Habari mbaya: Baba na mama watelekeza watoto wao ndani ya nyumba ....Mama kaolewa kwingine na baba kaoa kwingine

Image
KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida watoto wawili wenye umri wa miaka saba na nane wametelekezwa na wazazi wao kwa muda wa miezi mitano bila huduma za msingi. Watoto hao ambao wamefahamika kwa majina ya Agustino Steven (8) na Rebeka Steven(7) ni wanafunzi wa darasa la kwanza shule ya msingi Mapambano iliyopo Kata ya Iyela Jijini Mbeya. Wakizungumza kwa nyakati tofauti , watoto hao wamesema Wazazi wao waliwaacha kwenye nyumba ya kupanga tangu mwezi wa Mei mwaka huu ambapo Baba inasadikika alielekea Umalila Mbeya Vijijini ambako inasemekana ameoa mke mwingine. Wamesema Mama yao alielekea Mbozi ambako pia naye inasadikika ameolewa na mwanaume mwingine hivyo kuwaacha watoto bila kuwa na huduma za msingi kama Chakula na mavazi huku wakiwa wameachiwa nyumba mtaa wa Jakaranda Airport. Watoto hao waligundulika baada ya kukutwa mitaani wakitafuta riziki kwa kuzoa taka kwenye majumba ya watu kisha kupeleka majalalani kwa ujira wa kati ya shilingi 200 na 500 ambazo huzitumia kunun

HOUSIGELI (Mfanyakazi wa ndani ) amnyonga mtoto na kumtupa kwenye dimbwi la maji machafu

Image
Hausigeli aliyejulikana kwa jina moja la Ester (14) yupo matatani kwa madai ya kumuua mtoto Arafat Allan (3) kwa kumnyonga shingo na kumpiga na kitu kizito kichwani kisha kuutumbukiza mwili wake kwenye dimbwi la maji machafu. Tukio hilo lilijiri Jumapili iliyopita Mailimoja, Kibaha mkoani Pwani ambako marehemu alikuwa akiishi na wazazi wake. Akizungumza kwa uchungu, mama mzazi wa mtoto huyo, Zakia Peter ambaye amelazwa katika Zahanati ya Kellen kutokana na mshtuko wa kifo cha mwanaye, alisema siku ya tukio, hausigeli huyo aliyekuwa na siku mbili tangu aanze kazi aling’ang’ania kutumwa sokoni saa mbili asubuhi ambapo alimkubalia na kumuagiza mboga. AONDOKA NA MTOTO Bila mwanamke huyo kujua, msichana huyo alimpitia Arafat kwa jirani alikokuwa akicheza na wenzake na kuondoka naye kwa madai anamsindikiza. “Nilipoona muda unasonga mbele bila hausigeli kurudi na mtoto nilianza kuwatafuta,” alisema mama wa marehemu. Akasema aliwatafuta kwa muda mrefu bila mafanikio mwisho

ADAM MCHOMVU "(mtangazaji)awakwaza watu kwa kuweka picha yake mtandaoni akitiririsha KAMASI"

Image
Kupitia Account yake ya mtandao wa kijamii wa Instagram Mtangazaji wa Clouds Fm Adam amepost picha hii .Ni picha ambayo imezua gumzo sana miongoni mwa mashabiki wake... Wapo wanaohoji UTIMAMU wa akili yake kwa kuweka picha kama hiyo huku wengine wakidai ni bangi zinamsumbua..... Yafuatayo ni baadhi ya maoni ya mashabiki wake: