BREAKING : MBUNGE WA JIMBO LA SONGEA MJINI AFARIKI DUNIA

Taarifa zimetufikia asubuhi hii,zikieleza kuwa aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Songea Mjini,Mh Leonidas Gama amefariki Dunia usiku wa kuamkia leo.Mbunge wa Songea Mjini Leonidas Gama amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya Peramiho alikokuwa anapatiwa matibabu. Marehemu alipata kuwa Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro na Mkuu wa wilaya kadhaa zikiwemo Ilala, Muheza, Nachingwea, Newala na Mbeya.Tunaendelea kufuatilia kwa ukaribu zaidi wa taarifa hiyo.MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI-AMINA

Comments

Popular posts from this blog