RC Makonda Amshukuru Wolper

wolperPicha inayomuonesha Wolper akiwa amevaa fulana hiyo.
DAR ES SAALAM: Mkuu wa Mkoa wa Dar es Saalam, mheshimiwa Paul Makonda amemshukuru mwanadada Jaqueline Massawe ‘Wolper’ ambaye ni muigizaji anayefanya vizuri kwenye tansia ya Bongo Muvi nchini.
Mkuu huyo wa Mkoa amemshukuru muigizaji huyo kupitia akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Instagram baada ya Wolper kuweka picha kwenye akaunti yake ya Instagram akiwa amevaa fulana nyeupe yenye ujumbe wa kuhamasisha kampeni ya upandaji miti jijini Dar es Saalam itakayofanyika Oktoba Mosi, 2016.
Kampeni hiyo inayokwenda kwa jina la ‘Mti Wangu’ inasimamiwa na Mkuu wa Mkoa mh. Paul Makonda.
Mkuu wa Mkoa ameandika ujumbe huu kwenye akaunti hiyo unaosomeka:
“Huwezi kujuwa umeugusa Kwa kiasi gani moyo wangu. Wewe na watu wote wanao support campaign ya MTI WANGU. Niwashukuru sana sana.
“Endeleeni kuiunga Mkono serikali kwani miti tunayoipanda inafaida kubwa sana kwetu sisi Wananchi.”

Comments

Popular posts from this blog