Posts

Alichokisema Zitto Kabwe Baada ya Rais Kikwete Kuhutubia Bunge La Katiba

Image
Kupitia ukurasa wake wa facebook Zitto  Kabwe     ameandiki hivi;Serikali 2 zitaendeleza hisia za Utanganyika kwa kasi Mkuu wa Nchi kamaliza kuhutubia Bunge la Katiba. Kimsingi kaegemea upande wa msimamo wa Serikali 2 ambao ndio msimamo wa CCM chama anachoongoza. Hata hivyo kasisitiza kuwa iwapo tunataka Serikali 3 basi tuzingatie hofu zilizopo ikiwemo masuala ya Uraia, uwezo wa kifedha wa Serikali ya Muungano nk. Ni dhahiri kero za Muungano zilizodumu kwa z aidi ya miaka 50 haziwezi kutatuliwa na muundo ule ule uliozitengeneza.  Jawabu la muungano wa Tanzania ni muundo wa Serikali tatu wenye Serikali ya Muungano yenye nguvu na rasilimali. Tunaloweza kuongeza ni kuweka mfumo wa Tawala za Mikoa wenye kupanua demokrasia zaidi kwa kuchagua wakuu wa mikoa na kufuta wakuu wa wilaya. Ni dhahiri Uraia itakuwa ni 'deal breaker' kwenye suala la muundo wa Muungano. Hili litajibiwa kwa kuwa na Nchi moja, dola moja na Serikali tatu. ...

KAULI YA MADEE NA BABU TALE VIONGOZI WA TIP TOPBAADA YA DOGO JANJA KUOMBA MSAMAHA ILI ARUDI TIP TOP

Image
Baada ya Dogo Janja kuuomba msamaha kupitia vyombo vya habari uongozi wa Tip Top Connection na Madee aliyemtoa Arusha, Boss wa Tip Top Connection Babu Tale ameiambia tovuti ya Times Fm kuwa anataka rapper huyo aseme ukweli wa yote aliyoyasema awali baada ya kutoka Tip Top. “Babu Tale ameweka wazi vipengele ambavyo anataka Dogo Janja aviweke sawa. “Dogo anatakiwa aseme kama kweli aliibiwa, kama kweli alidhurumiwa na kama kweli hajawahi kuishi nyumbani kwa Madee. Anatakiwa aongee dhahiri asifiche, aongee tu ukweli.” Babu Tale ameeleza. Amegusia pia tukio ambalo lilimsikitisha zaidi wakati Dogo Janja anafanya kazi akiwa chini ya menejimenti ya Mtanashati Entertainment. “Siku zote kwenye ukweli uongo hujitenga, wakati yuko South Africa alipost picha ‘ningekuwa Tip Top nisingefika huku’. Nilishangaa heeh huyu kutoka huko kijijini kwao alifanyaje hadi kufika hapa “Wazazi wake nao wakawa wamekubali uongo wa mtoto wao wakaanza kutuongelea na sisi maneno amba...

PADRI AKUTA TUNGULI KABURINI KWA NGWEA

Image
Padri wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Monica, Kihonda mkoani Morogoro, Octavian Msimbe akionyesha tunguli zilizozungushiwa sanda zilizokutwa kaburini kwa marehemu Ngwea.  Wakati hati ya kifo cha aliyekuwa rapa bora Bongo, marehemu Albert Keneth Mangweha ‘Ngwea’, ikiendelea kushikiliwa nchini Afrika Kusini alikokutwa na umauti mwaka jana, kwenye kaburi lake kumekutwa tunguli zilizozungushiwa sanda,  linakupa mchapo kamili.     Tunguli hizo zilikutwa Ijumaa ya wiki iliyopita na Padri wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Monica, Kihonda mkoani Morogoro, Octavian Msimbe ambapo ziliibua hofu miongoni mwa waumini wa kanisa hilo lililopo katika eneo hilo la makaburi. Marehemu Albert Keneth Mangweha ‘Ngwea’.   PADRI AKEMEA Awali, ilielezwa kuwa siku hiyo padri huyo alioteshwa ndoto usiku juu ya uwepo wa vitu vya ajabu katika makaburi hayo ndipo akakemea kabla ya kwenda kuvishuhudia asubuhi yake (Ijumaa iliyopita) huku paparazi wetu...

MEZA YETU YA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI TAREHE 22.03.2014

Image
  MAGAZETI YA UDAKU LEO   MAGAZETI YA MICHEZO NA BURUDANI  

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA,JAKAYA MRISHO KIKWETE, WAKATI WA KULIHUTUBIA BUNGE MAALUM LA KATIBA, TAREHE 21 MACHI, 2014, DODOMA

Image
Mheshimiwa Samuel Sitta, Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba; Mheshimiwa Dkt. Mohamed Gharib Bilal, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi; Mheshimiwa Mizengo Peter Pinda, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Mheshimiwa Maalim Seif Sharif Hamad, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar; Mheshimiwa Balozi Seif Ali Iddi, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mheshimiwa Anne Semamba Makinda; Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano; Mheshimiwa Pandu Ameir Kificho, Spika wa Baraza la Wawakilishi na Mwenyekiti wa Muda wa Bunge Maalum la Katiba ; Mheshimiwa Rashid Othman Chande, Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Mheshimiwa Othman Makungu, Jaji Mkuu wa Zanzibar; Viongozi Wakuu Wastaafu; Waheshimiwa Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba; Waheshimiwa Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba; Wageni waalikwa; Mabibi na Mabwana; Pongezi Nakushukuru s...

Rais Kikwete Alipowasili Viwanja vya Bunge Dodoma na kukagua Bwaride Maalum.

Image
Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Mh. Samuel John Sita akibadilishana mawazo    na Makamu Mwenyekiti wake nje wa Ukumbi wa Bunge Mjini Dodoma kabla ya Kuanza kwa uzinduzi wa Bunge Maalum uliofanywa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete.kushoto Katibu wacBunge Maalum Yahya Hamad Khamis. Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete akiingia ndani ya Viwanja vya Bunge kulihutubia Bunge Maalum la Katiba Mjini Dodoma leo. Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Tanzania Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride rasmi lililotayarishwa na Jeshi la Polisi kabla ya kuzindua Bunge Maalum la Katiba Mjini Dodoma.( Picha na Hassan Issa wa – OMPR ) Othman Khamis Ame Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibnar Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete amesema    Umma wa Watanzania utajaa matumaini endapo jukumu walilopewa wajumbe wa Bunge Maalum la Ka...