AMBAKA ASKARI MWENZAKE ‘AKIMRINGISHIA’ UUME MREFU
Luteni-Kanali Chris Davies anayeshitakiwa kumbaka askari mwanamke baada ya kupiga vileo na wenzake huko Canada.
Haya yalisema mahakamani ambapo Luteni-Kanali Chris Davies anashitakiwa kwa kumbaka askari ambaye ni mama wa watoto wawili na umri wa miaka 53 katika tukio linalodaiwa kufanyika huko Kingston, Ontario, Canada.
Davies
anasemekana kumwambia mwanamke huyo kwamba: “Nina uume wenye urefu wa
inchi nane (sentimita 20.3) ambao unaweza kuubomoa ulimwengu wako.”
Mwanamme huyo anadaiwa alimfuata mwanamke huyo hadi hotelini kwake baada ya mwanamkehuyo ‘kubugia’ pombe mbalimbali za kutosha walipokuwa askari hao na wenzao wakinywa vileo.
Davies
na mwanamke mwathirika walikuwa sehemu ya kundi la askari waliokuwa
wakinywa vileo baada ya gwaride maalum kwenye kambi ya kijeshi ya Fort
Frontenac (pichani).
Mwanamke huyo aliripoti tukio hilo polisi mjini Kingston, Ontario, nchini Canada ambapo askari hao walikuwa wameungana na wale wa Canada kuadhimisha Mapigano ya Tuta (Ridge) la Vimy katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia.
Comments
Post a Comment