HUMPHREY POLEPOLE ATOA MSIMAMO WAKEKUHUSU KATIBA MPYA

Aliyekuwa mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba ambaye kwa sasa ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Humphrey Polepole ameweka wazi msimamo wake kuhusu mchakato wa katiba mpya, na kusema kuwa hajalitelekeza suala hilo.

Humphrey Polepole akiwa Kikaangoni
Polepole aliyekuwa kwenye kipindi cha Kikaangoni cha EATV kupitia facebook.com/eatv.tv, katika mahojiano yake na East Africa Radio amesema kuwa mchakato wa kuipata katiba mpya kwa Tanzania uko kwenye mikono salama chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli, na kuwataka watanzania waiache serikali irekebishe kwanza baadhi ya mambo ili mchakato huo utakapoanza usikumbwe na vikwazo.
Polepole amesema kwa uzoefu wake kama mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyokuwa chini ya Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Warioba, anafahamu mambo ambayo watanzania waliyataka na kwamba mambo hayo ndiyo ambayo yameanza kutekelezwa na serikali ya awamu ya tano ikiwemo kuwa kujali utu, kudhibiti rasilimali za umma, kuwataka wabunge wakae majimboni n.k.
Katika hatua nyingine, Polepole amewataka wanasiasa kwa sasa waache kuzungumzia suala la Katiba na badala yake wazungumzie ufisadi ili kuongeza nguvu katika vita dhidi ya rushwa na ufisadi.

Comments

Popular posts from this blog