Mlela Kuoa Mwanamke Aliyemzidi Umri


STAA wa filamu Bongo, Yusuf Mlela ametoa kioja cha aina yake baada ya kufunguka kuwa akifika hatua ya kuingia kwenye ndoa anataka mwanamke atakayemzidi umri.

Tofauti na vijana wengine ambao wanapenda kuoa wake wadogo kwao, Mlela alisema anaamini mwanamke akimzidi umri ndoa itadumu na maisha yao yatakuwa mazuri kwani atakuwa tayari ameshakomaa kiakili na atakuwa na uwezo mkubwa wa kuiendesha familia.



“Nahitaji mwanamke anayenizidi umri na sitaki nimzidi mimi naamini huyo tutaelewana na ndoa itadumu, sitaki mwanamke ninayemzidi umri mimi maana itakuwa shida kwani sijapangilia hivyo,” alisema Mlela.
Na Gladness Mallya

Comments

Popular posts from this blog