NYUMBA ALIMOFICHWA ‘MO’ YAFAHAMIKA, NI MBEZI BEACH DAR
Kamanda wa Kanda Maalum Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa, akiongea na waandishi wa habari leo.
Akizungumza na waandishi wa habari leo, Kamanda wa Kanda Maalum Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa, ameonyesha nyumba hiyo ambayo watekaji hao waliikodisha kwa kupanga kwa kusaidiwa na mtu mmoja aliyemtaja kwa jina la Twalib Mussa.Kwa mujibu wa maelezo ya Mambosasa, kufuatana na uchunguzi uliofanywa kwa kumhusisha pia Twalibu, watekaji hao walitoka Afrika Kusini.
Mohammed Dewji ‘Mo”.
Akifafanua zaidi, Mambomsasa, alisema Twalibu ambaye ni dereva wa teksi na mwenyeji wa Tanga pamoja na kuwasaidia kupanga katika nyumba hiyo, ndiye aliyewasafirisha kutoka eneo watekaji walipomwacha Mo, viwaja vya Gymkhana, na kuwapeleka hadi kituo cha mabasi cha Ubungo ambako wanasemekana waliondoka na kwenda kusikojulikana.
Gari alilotumia Twalibu kuwasafirisha watu hao lina namba za usajili za T918 CCY.
Comments
Post a Comment