Naibu Meya, Madiwani CHADEMA Wajiuzulu Mbeya

IKIWA ni saa chache baada ya uongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) mkoani Mbeya kupendekeza kuwavua uanachama madiwani watatu wa chama hicho mkoani humo kwa utovu wa nidhamu waliouonyesha, madiwani hao wamejiuzulu nyadhifa zao hizo.
Madiwani hao na kata zao katika mabano ni Geofrey Kajigili (Sisimba), Newton Mwatuboje (Manga)na Hamphrey Ngalawa (Iwambi).
Madiwani hao wamejiuzulu leo Jumamosi  Julai 21, 2018 baada ya Mwenyekiti wa Chadema Mbeya Mjini, Obadia Mwaipalu,  kutangaza uamuzi huo  katika mkutano wake na waandishi wa habari na kubainisha kuwa  vikao halali vya chama vilivyoketi mara kadhaa kujadili hatua stahiki dhidi ya madiwani vimefikia uamuzi huo.
Amesema kutokana na utovu wa nidhamu, kukiuka katiba ya Chadema na kukaidi utekelezaji wa maazimio ya uongozi, wamepeleka mapendekezo yao kwa uongozi wa chama hicho Kanda ya Nyasa ili  hatua zichukuliwe.
Aliyekuwa Naibu Meya na Diwani wa Kata ya Nsalaga Mjini Mbeya, Mchungaji David Ngogo (Chadema), amesema wamefikia uamuzi huo akidai kupingana na viongozi wao baada ya kudaiwa kumwalika Naibu Spika, Dk. Tulia Ackson kuchangia ujenzi wa Shule ya Sekondari Uyole.

Comments

Popular posts from this blog