Madiwani wapita bila kupingwa Uchaguzi mdogo wa Udiwani- Mbulu.



 Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Mbulu ndugu Hudson S. Kamoga akisoma taarifa ya maamuzi ya rufaa za Wagombea Udiwani katika kata za Tumati na Hayderer.

Akiongea na vyombo vya habari hii leo ofisini kwake Msimamizi wa Uchaguzi  jimbo la Mbulu, ndugu Hudson Stanley Kamoga amewatangaza Madiwani wawili wa kata ya Tumati ndugu Paulo Emanuel Axwesso (CCM) na ndugu Justine Sidamuy Masuja Hayderer(CCM),wamepita bila kupingwa  baada ya Wapinzani wao kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kushindwa rufaa waliokata Tume ya Taifa ya Uchaguzi dhidi ya Uamuzi wa Msimamizi wa Uchaguzi.
 
Msimamizi msaidi wa jimbo la Mbulu ndugu Michael Faraay(wa kwanza kushoto) akiwa na mratibu wa uchaguzi ndugu Stedvant Kileo wakimsikiliza kwa makini msimamizi wa uchaguzi (hayupo pichani)wakati wakusoma maamuzi ya rufaa

Akitoa taarifa juu ya maamuzi ya rufaa hiyo iliyotolewa na tume ya taifa ya Uchaguzi,msimamizi wa uchaguzi halmashauri ya Wilaya ya Mbulu amesema amewaita wagombea kwa mujibu wa Sheria za Serikali za Madiwani Sura namba 292 na Kanuni za uchaguzi wa Serikali za Mitaa za mwaka 2015.
 
 Mgombea Udiwani kwa kwa chama cha demekrasia na maendeleo ndugu Zakaria k. Hhaynihhi( kata ya Tumati) akipokea barua ya maamuzi ya Tume baada ya kupingwa rufaa yake.


Mbulu ni miongoni wa Majimbo ya Uchaguzi yaliyotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa mujibu wa Sheria na Kanuni na mnamo tarehe 14 ilitangazwa kuwa siku ya Uteuzi katika kata hizo mbili na taratibu zilifanyika kama ilivyopangwa. Wanachama wanne toka vyama viwili vya siasa walichukua fomu na kurejesha kwa mujibu wa sheria  na kanuni za Uchaguzi.
 

Mshindi wa nafasi ya Udiwani kata ya Tumati ndugu Paulo E. Axwesso akipokea nakala ya barua toka tume ya Taifa ya Uchaguzi ikionesha majibu ya   rufaa iliyompa ushindi wa kupita bila kupingwa.

Aidha Kamoga  amesema kuwa baada ya wagombea wote wanne kuteuliwa, Wagombea wawili wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo  walipingwa kutokana na sababu mbalimbali za ukiukaji wa ujazaji fomu namba 8 na msimamizi alichukua hatua za kuwaondoa wagombea kwa mujibu wa sheria za uchaguzi.
 
 Mshindi wa nafasi ya Udiwani kata ya Hayderer ndugu Justine S. Masuja akipokea kwa furaha nakala ya barua toka tume ya Taifa ya Uchaguzi ikionesha majibu ya   rufaa iliyompa ushindi wa kupita bila kupingwa.
 
Wagombea hao walikata rufaa tume ya taifa ya uchaguzi na majibu hayo kurejeshwa ikionesha wagombea wote wawili kukataliwa, ikumbukwe pamoja na kuondolewa kugombea nafasi hizo, mgombea wa Uchaguzi kwa kata ya Hayderer kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo alishatangaza kujiondoa kugombea nafasi hiyo kwa barua rasmi iliyo thibitishwa mbele ya mahakama.
 

Wagombea wa Uchaguzi wakiwa picha ya pamoja na wasimamizi wa uchaguzi hii leo mara baada ya kukabidhia majibu ya rufaa, kutoka kushoto ni mgombea udiwani CCM- Tuamati, Afisa uchaguzi, Msimamizi wa uchaguzi,mgombea udiwani kata ya Hayderer(CCM), Mratibu uchaguzi,na Mgombea udiwani Chadema- Hayderer
Uchaguzi mdogo wa Madiwani kwa kata mbili unafanyika kufuatia waliokuwa Madiwani wa kata hizo kujivua nafasi zao za uwakilishi wa Udiwani kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) na kuhamia Chama cha Mapinduzi(CCM) ili kuunga juhudi za Serikali ya awamu ya tano ya Mhe. John Pombe Magufuli  na kuacha kata zao wazi.

Baada ya  kuwatangaza rasmi Kamoga amasema utaratibu wa kuwakabidhi vyeti vya ushindi wa Udiwani zinaendelea na watakabidhiwa mnamo tarehe 12/08/2018 ambayo ilikuwa siku rasmi ya uchaguzi.


Comments

Popular posts from this blog