MZEE MWINYI AONGOZA SWALA YA EID EL FITR DAR

Mzee Ali Hassan Mwinyi akitoa nasaha zake kwa waumini wa dini ya Kiislamu.

Mzee Ali Hassan Mwinyi (kulia) akijumuika na waumini wengine wa Dini ya Kiislam katika 
swala ya Eid El Fitr iliyoswaliwa kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar esa Salaam.

Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Alhad Mussa Salum akitoa nasaha zake kwa waumini 
wa dini ya Kiislamu.

Taswira ya baadhi ya waumini waliojitokeza katika Viwanja vya Mnazi Mmoja ilivyoonekana.

Meneja wa Kampuni ya Global Publishers Ltd, Abdallah Mrisho (kulia) akiwa ameungana na 
waumini wengine wa Dini ya Kiislam katika swala ya Eid El Fitr iliyoswaliwa kwenye Viwanja 
vya Mnazi Mmoja jijini Dar esa Salaam.

Meneja wa Global Publishers, Abdallah Mrisho (katikati) akisalimiana na mmoja wa waumini 
baada ya kumalizika kwa swala ya Eid El Fitr.

Sehemu ya waumini akinamama waliojitokeza katika swala hiyo kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja.

Waumini wakiomba dua.

RAIS Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi, mapema leo Ijumaa amewaongoza waumini wa Kiislamu katika kusherehekea Sikukuu ya Eid El Fitr, katika swala ya Eid El Fitr  iliyofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waumini mara baada ya swala hiyo, mzee Mwinyi amewataka Waislamu  kote nchini kusherehekea sikukuu hiyo kwa kufanya matendo mema ya kumpendeza Mwenyezi Mungu na kuliombea taifa ili amani iliyopo iendelea kudumu milele.

“Waumini wa Dini ya Kiislam muendeleze ushirikiano,umoja na mshikamano na madhehebu mengine ya dini nchini, pia mwendeleze kudumisha matendo mema kama mlivyofanya kipindi cha mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani,”amesema.
source;GPL

Comments

Popular posts from this blog