Kufungiwa Nyimbo za Diamond Kwazua Gumzo Bungeni

Mbunge wa Viti Maalum (CCM) kupitia Vijana Mkoa wa ArushaCatherine Magige.
MBUNGE wa Viti Maalum (CCM) kupitia vijana Mkoa wa Arusha, Catherine Magige amehoji kufungiwa baadhi ya nyimbo za staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, wakati kamati ya maudhui ilikuwepo na kuziacha nyimbo hizo zikaenda hewani kwa muda mrefu.
Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’
Akijibu swali hilo, Waziri wa Habari , Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison  Mwakyembe,  amejibu kuwa Diamond siyo msanii wa kwanza kufungiwa nyimbo zake kwani hata wasanii wa Nigeria,  Davido na Wizkid,   wamefungiwa nyimbo  zao. Pia alimtaja mwanamuziki wa Jamhuri ya Kidemokrasiaya Congo, Kofii Olomide, ambaye wimbo wake  wa Ekoti Te umefungiwa nchini humo.
Pamoja na kuibuka wabunge wengi wenye kutaka kutoa taarifa na kuendelea hoja hiyo, Naibu Spika, Tulia Ackson,  hakuwapa nafasi.

Comments

Popular posts from this blog