MGUU WA MTOTO WANASA KWENYE NGAZI ZA UMEME AIRPORT
Mtoto
Julian ambaye mguu wake ulinaswa kwenye ngazi za umeme kwenye uwanja wa
ndege wa Vancouver, Canada. Mama yake, Andrea Diaczok, ametoa wito kwa
wazazi kuwa macho na watoto wao katika sehemu hizo.
Kiatu cha Julian kikiwa katika mashine za ngazi za umeme kilipokuwa kimenasa.
Julian akiwa amelazwa hospitali akipatiwa matibabu, kinyume na woga wa wazazi wake ambao walifikiri huenda mguu wake ungekatwa.
Wazazi wa Julian wakifurahi naye baada ya matibabu ya mguu wake ambayo yalichukua wiki kadhaa.
“Mtambo huo uliukunja mguu wake na kuvunja mifupa ya mguu ambapo kiatu chake kilipotelea ndani ya mkanda huo wenye kuzunguka,” alisema.
Kiatu cha Julian kilikuwa kimebanwa kwenye mkanda huo na ilibidi wafanyakazi wa uwanjani hapo na wapita njia kumng’oa mahali hapo aliponasa.
Diaczok na Lee ambao ni wafanyakazi katika fani ya afya, walikuwa wamejitayarisha kwamba mwanao angekatwa mguu. Hata hivyo, madhara hayakuwa makubwa sana, kwani mbali na mifupa iliyokuwa imevunjika na miteguko kadhaa, madaktari waliweza kuhakikisha mtoto huyo anapata matibabu ambayo hayakuwalazimisha kuukata mguu huo.
Comments
Post a Comment