Chuchu afunguka zawadi anayotaka kwa Ray

BAADA ya kumzalia mtoto wa kiume na kuwa gumzo mitandaoni, muigizaji mkongwe wa filamu Bongo, Chuchu Hans amefungukia zawadi aitakayo kutoka kwa mzazi mwenziye ambaye naye ni msanii, Vincent Kigosi ‘Ray’ kuwa ni busu tu.
Akizungumza na Star Mix, Chuchu alisema kuwa baada ya kumzalia Ray hahitaji kupewa zawadi kubwa kwani hata busu litamtosha.
“Unajua mimi nachojua zawadi ni zawadi tu hata kama Ray akiamua kunipa busu kwangu mimi linatosha kabisa wala asiwaze sana zawadi ya kunipa,” alisema Chuchu.

Comments

Popular posts from this blog