LEMA NA NASSARI WAANIKA USHAHIDI WA MADIWANI WA CHADEMA WALIVYONUNULIWA


Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari (Chadema) na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema wakijadiliana.
Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari (Chadema) na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, leo wamewasilisha ushahidi wa jinsi madiwani wa Chadema waliotangaza kukihama chama hicho na kuhamia Chama cha Mapinduzi (CCM), walivyohongwa ili wachukue uamuzi huo.
Wakizungumza na waandishi wa habari, Lema na Nassari wameonesha ushahidi wa video na sauti, ukiwahusisha mkuu wa Wilaya ya Arumeru, katibu tawala na mkurugenzi wa wilaya hiyo, walivyokuwa wakipanga michakato ya kuwanunua madiwani hao.
Kwa mujibu wa Lema na Nassari, madiwani hao, kila mmoja amepewa fedha ambazo walitakiwa kulipwa posho kwa vikao vyote walivyotakiwa kukaa mpaka 2020 wakiwa madiwani, wamesaidiwa miradi yao mbalimbali nakila mmoja amepewa shilingi milioni kumi.

see more at :- https://youtu.be/yTbqJUmZeag

Comments

Popular posts from this blog