Miili ya Ndugu 13 Waliofariki kwa Ajali Uganda Ilivyoagwa Dar (Pichaz)


Wanajeshi wa JWTZ wakibeba miili ya marehemu hao kupeleka eneo maalum kwa ajili ya kuaga.
SIMANZI, vivlio na majozni imetawala wakati wa kuaga miili ya Watanzania 13 ambao ni ndugu wa familia moja waliofariki kwenye ajali mbaya ya gari iliyotokea nchini Uganda hivi karibuni.

Waziri Angella Kairuki akiteta jambo na Betty Kamya ambaye ni mwakilishi wa Rais wa Uganda, Yoweri Museveni.
Miili ya wanafamilia hao imeagwa leo Septemba 20, 2017 katika Hospitali ya Jeshi la Wananchi ya Lugalo jijini Dar es Salaam na baadaye kusafirishwa kuelekea Arusha, Kilimanjaro na Mpwapwa kwa ajili ya mazishi.

Waombolezaji wakati wa shughuli ya kuaga marehemu.
Katika ibada hiyo ya kuwaaga marehemu, viongozi mbalimbali wa serikali walikuwepo wakiongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala), Angela Kairuki, Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles John Mwijage, Waziri Maalum wa Kusimamia Jiji la Kampala, Betty Kamya kutoka Uganda aliyemwakilisha Rais wa nchi hiyo, Yoweri Museveni kukabidhi miili ya marehemu kwa ndugu zao.

Majeneza yenye miili ya marehemu.
Aidha, Rais Museven ametuma salamu maalum za rambirambi ambazo zilisomwa na Betty kwa niaba yake na kupokelewa na Waziri Kairuki kwa niaba ya Rais Magufuli. 

Majeneza yenye miili ya marehemu.
Tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia Jumatatu, Septemba 18, 2017 katika eneo la biashara Lubanda takribani kilomita 80 kufika Kituo cha Polisi cha Fika Salama karibu na Mto Katonga Wilaya ya Mpigi, Kampala, Uganda. 

Ajali hiyo mbaya ilihusisha gari aina ya fuso yenye namba za usajili UAH 970P na coaster yenye namba T540 DLC waliokuwa wakitumia Watanzania hao waliokuwa wakitoka kwenye  harusi ya binti wa Dkt. Annette Ibingira ambaye ni mke wa mhazini wa shule ya Wazazi ya Kampala nchini Uganda Dkt. Ibingira.

Aidha Majeruhi wa ajali hiyo walipelekwa katika Hospitali ya Nkozi na Double Cure Clinic zilizopo nchini Uganda.

Tukio hilo lilimgusa pia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliyetumia salamu za rambirambi aliyewahi kuwa Naibu Waziri na Mbunge Mstaafu wa Jimbo la Mpwapwa Mkoani Dodoma Bw. Gregory Teu kufuatia vifo vya watu hao ambao ni ndugu wa familia yake.









Ndugu wakisaidiwa kuaga miili ya marehemu.

Comments

Popular posts from this blog