Miili ya Ndugu 13 Waliofariki kwa Ajali Uganda Ilivyoagwa Dar (Pichaz)
Wanajeshi wa JWTZ wakibeba miili ya marehemu hao kupeleka eneo maalum kwa ajili ya kuaga.
SIMANZI, vivlio na majozni imetawala
wakati wa kuaga miili ya Watanzania 13 ambao ni ndugu wa familia moja
waliofariki kwenye ajali mbaya ya gari iliyotokea nchini Uganda hivi
karibuni.
Waziri Angella Kairuki akiteta jambo na Betty Kamya ambaye ni mwakilishi wa Rais wa Uganda, Yoweri Museveni.
Waombolezaji wakati wa shughuli ya kuaga marehemu.
Majeneza yenye miili ya marehemu.
Aidha, Rais Museven ametuma salamu maalum za rambirambi ambazo zilisomwa na Betty kwa niaba yake na kupokelewa na Waziri Kairuki kwa niaba ya Rais Magufuli.
Majeneza yenye miili ya marehemu.
Tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia Jumatatu, Septemba 18, 2017 katika eneo la biashara Lubanda takribani kilomita 80 kufika Kituo cha Polisi cha Fika Salama karibu na Mto Katonga Wilaya ya Mpigi, Kampala, Uganda.
Ajali hiyo mbaya ilihusisha gari aina
ya fuso yenye namba za usajili UAH 970P na coaster yenye namba T540 DLC
waliokuwa wakitumia Watanzania hao waliokuwa wakitoka kwenye harusi ya
binti wa Dkt. Annette Ibingira ambaye ni mke wa mhazini wa shule ya Wazazi ya Kampala nchini Uganda Dkt. Ibingira.
Aidha Majeruhi wa ajali hiyo walipelekwa katika Hospitali ya Nkozi na Double Cure Clinic zilizopo nchini Uganda.
Tukio hilo lilimgusa pia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliyetumia salamu za rambirambi aliyewahi kuwa Naibu Waziri na Mbunge Mstaafu wa Jimbo la Mpwapwa Mkoani Dodoma Bw. Gregory Teu kufuatia vifo vya watu hao ambao ni ndugu wa familia yake.
Ndugu wakisaidiwa kuaga miili ya marehemu.
Comments
Post a Comment