RC Makonda ametangaza Walemavu DSM kupewa miguu ya bandia bure

Paul Makonda 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, akionyesha mfano wa miguu ya bandia leo jijini Dar es salaam.
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda amefanikiwa kupata miguu ya bandia itakayoweza kuwasaidia wananchi wenye mahitaji.
Miguu hiyo yenye thamani ya Shilingi Milion 800 itatolewa bila malipo kwa wananchi waliopata ajali na kushimdwa kupata miguu hiyo kutokana na kushindwa kumudu gharama za kununua miguu hiyo ambapo mguu mmoja unagharimu Milion tatu.
Kwa mantiki hiyo amewatangazia wananchi wote wenye mahitaji ya miguu ya bandia na hawana uwezo wa kumudu gharama kufika ofisini ya mkuu wa mkoa siku ya Jumatatu na Jumanne kwaajili kukutana na wataalamu wa miguu watakaochukua vipimo kwaajili ya kutengenezewa miguu kulingana na maumbile yao.
Amesema miguu hiyo ya watu 200 itatolewa kwa awamu hii ya kwanza ambapo kama mahitaji yatakuwa makubwa na wafadhili wakaongezeka itatolewa tena kwa awamu nyingine lengo likiwa ni kuwasaidia wananchi kutotumia magongo.
"Nimepewa kazi ya mkoa kuhudumia makundi yote, nafahamu kwenye mkoa wangu wapo waliopata ajali na wengine wakavunjika miguu lakini pesa ya kupata miguu ya bandia ili waachane na magongo kwao imekuwa ni moja ya changamoto, kutokana na sababu hiyo nimeona vyema nifikiri namna ya kuwasaidia wananchi ambao hawana uwezo ili waweze kupata, nimefanikiwa kupata wadau watakaonipatia miguu ya kuhudumia wananchi 200" Alisema Makonda.

Comments

Popular posts from this blog