Floyd Maywether amtwanga McGregor kwa TKO

 Baada ya tambo za bondia Conor McGregor kuelekea pambano dhidi ya Floyd Maywether ambaye hajawahi kupoteza pambano, asubuhi ya August 27 katika ukumbi wa  T-Mobile Arena mjini Nevada, USA majibu yalipatikana.

Mayweather alikuwa anaingia kucheza pambano lake la 50 dhidi ya McGregor ambaye yeye lilikuwa ni pambano lake la 25 akiwa ndio kapoteza kwa mara ya pili na kashinda mara ya 23, ushindi wa leo wa Mayweather unakuja baada ya kumpiga bondi wa Philipino Manny Pacquiao May 3 2015 kwa point mjini Las Vegas.

Bondia Floyd Mayweather leo ameshinda pambano lake la 50 akiwa kacheza mapambano 50 bila kupoteza, amefanikiwa kuendelea kutetea rekodi yake kwa kumpiga Conor McGregor kwa Technical Knock Out (TKO) katika round ya 10 pambano la round 12.

Comments

Popular posts from this blog