Serikali Yatoa Onyo kwa Wanaotumia Vibaya Mitandao ya Kijamii

SeeBait
Serikali imesema inajipanga kukabiliana na matumizi mabaya ya mtandao ikiwa ni pamoja na kuwachukulia hatua za kisheria wanaotumia vibaya.

Akizungumza katika majadiliano ya usalama wa mitandao ya kijamii kati ya Tanzania na China, Naibu Waziri wa Wizara wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Injinia Edwin Ngonyani amesema serikali itawachukulia hatua kali wanaotumia vibaya mitandao ya kijamii wakiwamo wanaotuma ujumbe wenye dhamira ya kuwachafua wengine. Kwani Tanzania bado inakabiliwa na changamoto ya udhibiti wa usalama wa matumizi ya mitandao ya kijamii.

“Tanzania bado iko nyuma katika masuala ya kudhibiti usalama wa matumizi ya mitandao kama vile Twitter, Facebook, Instagram na YouTube, wenzetu China wamefanikiwa kudhibiti suala hilo,” amesema Injinia Ngonyani.

Naibu Waziri wa Udhibiti wa mtandao wa China, Ren Xianliang alisema nchi yao imefanikiwa kwa kiwango kikubwa katika kudhibiti matumizi ya usalama wa mtandao kwa kuwa walianzisha mtandao wao ambao umekua anasaidia kufuatilia masuala ya nchi yao vikiwamo vivutio mbalimbali ambavyo huwashawishi na kutoa hamasa kwa wananchi wengi kuweza kutumia mtandao huo.

“Sisi katika kudhibiti matumizi ya usalama wa mitandao ya kijamii katika nchi yetu tumefanikiwa kwa kiwango kikubwa Kutokana kuanzisha mtandao maalumu ambapo tumekua tukifanya vipindi mbalimbali vya kuhamasisha na kuwashawishi wananchi kutumia mtandao huo,” alisema Xianliang.

Comments

Popular posts from this blog