IGP SIRRO ALIPONGEZA JESHI LA POLISI MKOA WA SINGIDA

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro akipiga saluti wakati wa paredi ya polisi iliyoandaliwa lililoandaliwa kwa ajili yake kulikagua mapema leo kwenye viwanja vya kambi ya FFU mjini hapa.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro akikagua baadhi ya askari wa jeshi la polisi mjini Singida leo piga saluti wakati wa paredi ya polisi iliyoandaliwa lililoandaliwa kwa ajili yake kulikagua.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada kukagua askari polisi waliokuwa kwenye paredi kwenye viwanja vya kambi ya FFU mjini hapa.

………………………….

Picha/Habari na Gasper Andrew.
Mkuu wa Jeshi la polisi nchini (IGP), Simon Sirro amelipongeza jeshi la polisi Mkoani Singida kwa juhudi zake za kupunguza matukio ya uhalifu yakiwemo ya utekeji wa magari kwa kiwango kikumbwa.IGP Siro ametoa pongezi hizo leo asubuhi alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kweye viwanja vya kambi ya kikosi cha kuzuia fujo (FFU) mjini hapa.Amesema matukio ya uhalifu mbalimbali mkoani Singida yamekupungua kwa kiwango kikubwa kwa sasa, ikilinganishwa na miaka ya nyuma.“Hatua hii inachangia uwepo wa amani na utulivu kwa wananchi wa mkoa wa Singida hivyo kutoa fursa kuweza kujiletea maendeleo yao ya mkoa na taifa kwa ujumla” amesema.
IGP Siro amesema mafanikio hayo yamechangiwa na wananchi kwa kiwanngo kikubwa kwa kutoa ushuirikiano kwa jeshi la polisi. Akifafanua amesema wananchi wamekuwa wakitoa taarifa sahihi na kwa wakati kwa jeshi la polisi pindi wanapobaini dalili ama matukio ya kihalifu.“Kwa sasa kwa kweli wananchi hata ninyi waandishi wa habari mnatupa ushirikiano mzuri sana. Ushirikiano huu unachangia kazi zetu kuwa nyepesi na za mafanikio makubwa. Sasa hivi kule Kibiti mkoani Pwani, wananchi wanatusaidia mno taarifa zinazohusu mauaji ya watu wasiokuwa na hatia”, amefafanua zaidi.IGP Siro amesema kwa sasa Tanzania inaonewa wivu na nchi jirani kwa namna tulivyo dhibiti matukio ya kihalifu na kupelekea nchi kuendelea kudumisha amani na utulivu.
Wakati huo huo, Mkuu huyo wa jeshi la polisi ametumia fursa hiyo kuwaomba wananchi waendelee kushirikiana na jeshi hilo, kufichua baadhi ya watu wanaojihusisha na matukio mbalimbali ya kihalifu ili waweze kuchukulia hatua stahiki.

Comments

Popular posts from this blog