Pogba kutua Tanzania

Klabu ya Everton inajiandaa kuja nchini Tanzania kwa ziara ya kujiandaa na msimu ujao wa ligi ambapo wakiwa hapa wtacheza na washindi wa kombe la Sports Pesa timu ya Gor Mahia kutoka nchini Kenya.
Sasa Everton wanaweza kuja na Pogba nchini Tanzania kama dili lake la usajili kujiunga nao likikamilika kabla hawajaja Tanzania, tetesi zinasema Everton wanajaribu kumsajili Florentin Pogba kutoka katika klabu ya St Etienne.
Taarifa kutoka nchini Ufaransa zinasema timu za Everton na Red Bull Leipzig zote zinapambana kumnunua mlinzi huyo wa kushoto mwenye umri wa miaka 26 lakini Everton wanapewa nafasi kubwa kwani Florent anatamani kucheza ligi moja na Paul Pogba.
Katika msimu uliopita wa ligi mlinzi huyo amecheza michezo 17 tu na alishacheza dhidi ya Paul Pogba msimu uliopita katika michuano ya Europa na jarida la Jeune Afrique limeshatabiri kwamba Florent anaweza kuitosa Red Bull na kujiunga na Everton.

Comments

Popular posts from this blog