MSANII ESTER APANGIWA MJENGO NA MWANAUME

MSANII wa filamu za Kibongo, Ester Kiama anadaiwa kupangishiwa mjengo na mwanaume ambaye ni mume wa mtu aliyemhamisha ku­toka Kijitonyama alikokuwa anaishi na kumwamishia Mbezi Beach.

Chanzo makini kilieleza kuwa kwa sasa Ester anaishi kwenye nyumba nzima yenye hadhi tofauti na alikokuwa akiishi mwanzo ambapo amelipiwa kodi ya mwaka mzima na mwanaume huyo.
Risasi Jumamosi lilimtafuta Ester ili kujibu tuhuma hizo na alipopatikana alikiri kuhamia Mbezi Beach kwenye nyumba ny­ingine nzima lakini ali­pinga suala la kupang­ishiwa na mwanaume.
“Ninaishi Mbezi Beach kwa sasa amba­ko nimehamia hivi kari­buni, habari za kwamba nimelipiwa kodi na mwanaume ni uongo, nimejilipia mwenyewe,” alisema Ester.


Comments

Popular posts from this blog