Kilichouzwa nje ni Madini, Sio mchanga

 "Biashara ya uuzwaji wa Makinikia haikufanyika kwa ushindani na si kweli kwamba wanauza Makinikia, kinachouzwa ni madini." amesema Mwenyekiti wa Kamati ya kuchunguza mchanga wa madini, Profesa Nehemiah Osoro
Prof. Osoro ameyasema hayo wakati akikabidhi ripoti ya kamati yake kwa Rais John Magufuli leo katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam.
Amesema kuwa gharama za shughuli za utafutaji na upembuzi madini nchini zimejumuishwa katika mauzo yake kwa kupunguza faida hivyo hawatozwi kodi.
"Faida yote iliyopatikana katika uuzwaji wa dhahabu nje haikujumuishwa katika mahesabu ili kukwepa malipo ya mrabaha" alisema Prof. Osoro
Ameongeza kuwa uchunguzi wa kamati yake umebaini kuwepo kwa utakatishwaji haramu wa fedha na faida kurudishwa kama mkopo kwa makampuni ya madini kitu ambacho ni kinyume cha taratibu.

Comments

Popular posts from this blog