GONJWA LA ZARI THE BOSS LADY HOFU YATANDA,SIKU CHACHE MUMEWE KUFARIKI

PRETORIA: Takriban siku 25 baada ya kifo cha aliyekuwa mumewe, Ivan Ssemwanga ‘Don Ivan’, staa wa Afrika Mashariki, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, ameibua hofu kubwa kwa ndugu, jamaa na marafi ki baada ya kupata gonjwa la ghafla lililosababisha kukimbizwa hospitalini akiwa hoi.Kwa mujibu wa mpenzi wake ambaye ni msanii wa Bongo Fleva, mapema wiki hii, Zari alikimbizwa hospitalini huko Pretoria nchini Afrika Kusini na kulazwa kutokana na hali yake kuwa mbaya. Ilifahamika kwamba, Zari alikutwa na hali hiyo siku moja tu tangu mama yake mzazi, Halima Hassan naye alazwe jijini Kampala, Uganda kwa matatizo ya moyo kushindwa kufanya kazi hivyo kupishana kwa saa kadhaa za kukimbizwa hospitalini.

NI SIKU CHACHE TANGU AKABIDHIWE OFISI YA IVAN
Ilielezwa kwamba, Zari ambaye ni mfanyabiashara wa Uganda mwenye makazi Afrika Kusini alikutwa na hali hiyo ikiwa ni siku chache tangu alipoanza kufanya kazi kwenye ofi si ya Ivan aliyokabidhiwa hivi karibuni huko Pretoria, Juni 15, mwaka huu. Hata hivyo, habari hizo hazikueleza ni nini hasa kinachomsumbua Zari hadi kuwa katika hali hiyo hivyo ndugu, jamaa na marafi ki kupata hofu kubwa.
Katika hofu hiyo, baadhi ya ndugu hao walikaririwa wakisema kwamba, kutokana na mbilingembilinge za msiba wa Ivan ambapo Zari alikuwa ndiye kila kitu, ilikuwa ni lazima aumwe kwa kuwa alichoka mno. “Ukiacha uchovu lakini pia maumivu ya majonzi ya kufi wa na baba watoto wake vinaweza vikawa vimechangia kupata gonjwa ambalo hadi hivi sasa halijajulikana,” alikaririwa mmoja wa ndugu wa mpenzi wake wa sasa wa jijini Dar.

KUHUSU MAMA YAKE
Habari kutoka Kampala zilieleza kuwa, wakati Zari akiwa bado mambo hayajakaa sawa, mama yake huyo aliugua ghafl a hivyo kulazimika kukimbizwa hospitali usiku.

“Ndiyo, mama Zari alikimbizwa hospitalini usiku lakini Zari hakuposti chochote kuhusu hilo.

NDUGU WA KARIBU ATOA HABARI
“Lakini ndugu wa karibu wa Zari ndiye aliyetoa habari kuhusu mama yake akisema kuwa, alikimbizwa hospitalini na kubainika kuwa ana tatizo la moyo kushindwa kufanya kazi,” kilikaririwa chanzo cha habari nchini Uganda na kuongeza: “Mama yetu amelazwa hospitali kutokana na tatizo hilo, anahitaji maombi yako.
Insha’allah atapona…” Hadi gazeti hili linakwenda mitamboni, hakukuwa na taarifa za wawili hao kuruhusiwa kutoka hospitalini hivyo bado ndugu, jamaa na marafi ki wana hofu juu ya mwanamama huyo na mama yake.
Zari ambaye ndiye msimamizi wa biashara kibao alizoziacha Ivan, ameachiwa watoto watatu wa kiume aliozaa na Ivan, Pinto, Raphael na Quincy ambapo ana wengine wawili, Tiffah na Nilan aliozaa na mpenzi wake wa sasa hivyo kuwa na jumla ya watoto watano.

NA MWANDISHI WETU, AMANI
GPL

Comments

Popular posts from this blog