MREMBO ALIPIA BANGO KATIKATI YA JIJI AKITANGAZA KUWA BIKIRA,ADAI ANASAKA TENDO KABLA HAJAFA

Katika hali isiyo ya kawaida, muigizaji wa vipindi vya TV mwenye umri wa miaka 40 amelipia ‘Bango’ kubwa katikati ya jiji akijitangaza kuwa ni bikira anayetafuta mwanaume wa kufanya naye tendo la ndoa ili asife bila kujua uhondo wake.Kwa mujibu wa Daily Mirror, Aranya ‘Pui’ Pathumthong ambaye ni muigizaji wa Thailand, aliyeweka bango hilo katika jiji la Bankok, karibu na wilaya ya Lat Phrao amesisitiza kuwa yuko ‘serious’ na tangazo hilo ambalo ameliweka baada ya matangazo yake kupitia mitandao ya kijamii ya mahusiano nchini humo kushindwa kuzaa matunda.
Tangazo lake limeandikwa, “I Want You. “40 and a virgin. Pui Aranya is looking for a husband!”Let me get it once before I die.” Linaonesha namba ya simu pia.Aranya ameviambia vyombo vya habari nchini humo kuwa ameamua kusaka mwanaume kwa mtindo huo ili aweze kuonja raha ya penzi kabla hayafa.Hata hivyo, Polisi jijini humo wameamuru Bango hilo liondolewe ingawa limelipiwa na kuongeza kuwa wanahitaji kumhoji mwanamke huyo kuhusu uamuzi wake wa kuweka bango hilo.

Comments

Popular posts from this blog