MENEJA BABU TALE AFUATA NYAYO ZA DOGO JANJA

Baada ya hitmaker wa ngoma ya Kidebe, Dogo Janja kutamba katika mitandao ya kijamii siku chache zilizopita huku akijitapa kuwa yeye ndio msanii ambaye anapendeza kuliko wote hapa Tanzania, round hii ni zamu ya meneja wa Tiptop Connection na WCB Hamisi Tale a.k.a Babu Tale.
Jana kupitia ukurasa wake wa Instagram Babu Tale alipost picha iliyomuonyesha akiwa na Dogo Janja na kuandika caption ambayo iliwaacha wengi midomo wazi.
Caption ya Babu Tale ilisomeka kama “Mpuuzi atabisha mimi ndio Manager wa kwanza Tanzania nzima kwa kupendeza na niko na msanii kwa kupendeza @dogojanjatz”

Comments

Popular posts from this blog