BREAKING NEWS:WATU WANNE WAFUKIWA NA KIFUSI DAR NA MMOJA AFARIKI DUNIA


Watu wanne wameripotiwa kufukiwa na kifusi katika machimbo ya kokoto, Golani yaliyopo eneo la Pugu nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
DC wa Ilala, Sophia Mjema akizungumza na wanahabari eneo la tukio.
Kwa mujibu wa Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema amesema kuwa, tukio hilo lilitokea jana Alhamisi majira ya saa 8 mchana ambapo ameeleza kuwa mpaka sasa vyombo vya uokoaji vimefanikiwa kupata watu wawili ambapo mmoja alikuwa tayari amekwishafariki dunia.
Mjema ameeleza kuwa mwili wa marehemu umehifadhiwa katika katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na mtu wa pili  aliyeokolewa akiwa hai alikuwa amevunjika mguu ambaye pia amepelekwa Muhimbili kwa ajili ya kutibiwa.
Aidha DC Mjema ameeleza kuwa, wawili waliobakia hawajafanikiwa kuokolewa kutokana na changamoto ya mvua nyingi zinazoendelea kunyesha pamoja na ubovu wa miundombinu ya njia za kupitishia mitambo ya uokoaji.
Eneo la machimbo hayo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Ilala, Salumu Hamduni amesema kuwa, wanachokisubili mpaka sasa ni mtambo maalumu kwa ajili ya ukoaji. Taratibu za kufukua miili ya watu iliyobaki ndani ya kifusi bado inaendelea.
DC Sophia Mjema akitoa maelekezo, ambapo nyuma yake kushoto ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Ilala, Suleiman Hamduni.

Comments

Popular posts from this blog