KESI INAYOMKABILI MAXENCE MELO YAAHIRISHWA TENA HADI APRILI 3

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imesema kesi namba 456 inayomkabili Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Jamii Forums, Maxence Melo na mwenzake na Mwanahisa Mike Mushi isipoendelea itafutwa.

Hayo yalisemwa alhamisi hii na Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba baada ya kukerwa na upande wa Jamhuri ambao ulishindwa kuwasomea washtakiwa maelezo ya awali badala yake ukaomba kuahirisha kesi.
Mwendesha Mashtaka, Inspekta Hamis Said, alidai mbele ya Hakimu Simba kwamba kesi ilitakiwa kuanza kusikilizwa awali lakini wakili anayeiendesha anaumwa. Mwendesha mashtaka aliomba kesi hiyo iahirishwe mpaka tarehe nyingine itakayopangwa.
Hata hivyo Hakimu Simba alieleza kukerwa na tabia ya kesi kuahirishwa na kusema wakati mwingine kama kesi hiyo haitaendelea ataifuta. Aliahirisha kesi hiyo hadi Aprili 3, mwaka huu na dhamana ya washtakiwa inaendelea.
By: Emmy Mwaipopo

Comments

Popular posts from this blog