RC MAKONDA AELEZA KILICHOMFANYA ATAJE MAJINA YA WATUHUMIWA WA DAWA ZA KULEVYA

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema kuwa uamuzi wa kuwataja hadharani majina ya watuhumiwa wa biashara ya dawa za kulevya ni kutokana na maombi ya Watanzania waliyayotoa wakati wa serikali ya awamu ya nne.


Makonda alisema kuwa licha ya watu wengi kupaza sauti zao wakitaka watuhumiwa wa dawa za kulevya watajwe hadharani, lakini Rais Mstaafu, Dkt Jakaya Kikwete yeye hakuwataja huku akiacha vyombo husika vifanyekazi zao kwa usiri.


Lakini kwa upande wa serikali ya awamu ya tano, waliamua kuwataja watuhumiwa hao ikiwa ni kujibu maombi ya kile watanzania walichokitaka tangu kipindi cha nyuma, alisema Makonda jana akiwa kwenye semina ya Walimu Wanaosomesha Quran Tanzania (JUWAQUTA).


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akizungumza katika unafunguzi semina ya Walimu wanaosomesha Qur-an Tanzania (JUWAQUTA) leo jijini Dar es Salaam.

“Mzee Jakaya mlimpigia kelele taja, taja, taja, taja, sasa tulipoingia sisi tukaona wacha tufanye kama alivyokuwa mnataka” alisema RC Makonda.
Aidha, RC Makonda amewakosoa wote walioibuka na kumdhihaki sababu alitaja majina hayo akisema kuwa giza haliwezi kuondolewa kwa giza bali ni kuwaleta waliopo gizani kwenye nuru.
“Uliona wapi giza linaondolewa kwa kutumia giza? Aliyefanya mafichoni anawekwa hadharani na harudii tena,” alisema Makonda.
Katika awamu ya tatu ya vita dhidi ya dawa za kulevya, RC Makonda hakutangaza majina hadharani kama alivyofanya katika awamu mbili zilizopita ambapo alimkabidhi majina 97, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya Rogers Sianga ili ayashughulikie.

Comments

Popular posts from this blog