WAJIUA HUKU WAKIJIREKODI FACEBOOK

Jay Bowdy (Kushoto) na Nakia Venant (Kulia). 
MWANAUME mmoja nchini Marekani anayejulikana kwa jina la Jay Bowdy, 34, ambaye pia ni muigizaji chipukizi amekutwa akiwa amejiua garini huku taarifa zikisema kwamba kabla ya kujiua, aliwaambia wafuasi wake kwenye Mtandao wa Kijamii wa Facebook kwamba anajiua hivyo wawapigie simu polisi kutoka hapo Los Angeles na kuwaambia kwamba alikuwa akijiua. 
Baada ya kupewa taarifa na raia wema, polisi kutoka katika kituo kikuu hapo Los Angeles walijaribu kumpigia jamaa aliyelipaki gari lake katika ya Mitaa ya Cumpston na Fulcher lakini hawakuweza kumpata kwa kuwa tayari alikuwa amekwishatekeleza kile alichokitaka. 
Watu waliokuwa wakifuatilia tukio hilo katika video hiyo iliyokuwa ikirekodiwa ‘live’ walipigwa na bumbuwazi kwani wengi walihisi kwamba alikuwa akiigiza kutokana na kazi yake hiyo kumbe mshikaji alikuwa akijiua kweli. Baadaye video hiyo ikatolewa mtandaoni na Facebook. 
SABABU YA KUJIUA 
Chanzo kilichokuwa hapohapo Los Angeles kinasema kwamba inawezekana Jay mwenye watoto wanne alijiua baada ya kupata msongo wa mawazo kwani alikuwa akikabiliwa na kesi ya kumdhalilisha kijinsia mwanamke mmoja huku akitakiwa kumlipa kiasi cha dola laki moja ambazo ni zaidi ya shilingi milioni 200. 


MWINGINE NAYE AJIUA 
Huku zikiwa hazijapita hata saa 12, msichana mmoja, Nakia Venant ‘14’ anayeishi Jijini Miami alifanya kama alivyofanya Jay kwa kujirekodi akiwa bafuni na kisha kujiua kwa kujinyonga kwa kutumia taulo lake alilolifunga bafuni mapema wiki hii. 
Kifo cha Nakia kimezua hofu kwa wazazi wa maeneo hayo na polisi wa Jimbo la Florida wamesema kwamba wanaendelea kuchunguza kifo cha msichana huyo ambacho kimeonekana kuwa cha kipekee kwa kitendo cha kujirekodi ili wafuasi wake watazame anavyokufa.⠀ 
Mtu aliyeona tukio hilo na kumtambua mhusika alikuwa rafiki wa msichana huyo ambapo mara moja akawataarifu polisi na kuwaeleza kilichokuwa kikiendelea ambapo mpaka polisi wanafika eneo la tukio, tayari Nakia alikuwa amekwishafariki dunia. 
Polisi hao wamewaambia waandishi wa habari kwamba kilichowafanya kuchelewa kufika huko ni kwamba rafiki wa Nakia alikosea kuwapa anwani ya kufika huko, kitu kilichowafanya kupotea, mpaka wanapata anwani yenyewe, wakawa wamekwishachelewa kufika huko kwa wakati

Comments

Popular posts from this blog