JESHI LA POLISI KANDA MAALUM YA DAR ES SALAAM LIMEKAMATA MAGARI MATANO.


Kamishina wa Polisi wa kanda maalm ya Dar es Salaam CP Saimon Sirro akizugumza na waandishi wa habari juu ya Jeshi la polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam kuhusu kukamata magari matano ambayo yanasadikiwa kuwa yaliibiwa katika vipindi tofauti katika maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam. Picha na Emmanuel massaka, Globu ya jamii.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi (CP), Simon Sirro akionyesha silaha aina ya SHORTGUN PUMP ACTON iliyo kutwa nyumbani kwa mtuhumiwa huko Boko njiapanda leo jijini Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi (CP), Simon Sirro akionyesha kadi bandia za chanjo ya homa ya manjano zilizokamatwa maeneo ya Hospital ya Mnazi mmoja jiji Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi (CP), Simon Sirro akionyesha magari yaliyokuwa yameibiwa katika sehemu mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam leo. Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi (CP), Simon Sirro akionyesha mitambo ya kutengenezea Gongo jijini Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi (CP), Simon Sirro akionesha mkasi wa kuvunja.
Jeshi la polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam limekamata magari matano ambayo yanasadikiwa kuwa yaliibiwa katika vipindi tofauti katika maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari Kamishina wa Polisi wa kanda maalm ya Dar es Salaam CP Saimon Sirro amesema kuwa mnamo Januari 22 mwaka huu jeshi la polisi lilikamata gari aina ya Toyota karina lenye namba za usajili T 950 DFN baada ya msako wa jeshi hilo katika maeneo ya Bandari jijini Dar es salaam.
‘’Gari jingine ambalo tumelikamata Toyota landcruseir Prado lenye namba zasajili T 959 DFT gari hili katika uchunguzi wetu liliibiwa September 16 mwaka jana na badaye kuonekana maeneo ya Mwanza januari 21 Mwaka huu’’ Alisema Kamishina Simon Sirro.
Kamishina Sirro amesema kuwa jeshi hilo pia limewakamata watuhumiwa kwa wizi wa pikipiki katika maeneo mbalimbali ya jijini Dar es salaam na Pwani pamoja na mkoa wa Morogoro baada ya operesheni iliyofanywa na jeshi hilo .
Amesema kuwa jeshi hilo limewakata vinara saba wa utengenezaji wa kadi bandia za chanjo ya homa za manjano ambapo huziuza kwa watu wanaofika katika hospitali ya Mnazi moja kwaajili ya kupata huduma za matibabu kabla yakusafiri nje ya nchi.
‘’Baadhi yawatuhumiwa waliokamatwa ni pamoja na Aisha Hassani(29) mkazi wa Vingunguti, Yakobo Msenga (42) mkazi wa Chanika, Oliver Bwegege mhamasishaji (58) mkazi wa Kigogo’’ Ameongeza Sirro.

Comments

Popular posts from this blog