Papa Francis Awatembelea Waliokua Makahaba Zaidi ya 20 Roma

Pope francis (4)
Roma, Italia
Kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis amewashangaza makahaba wa zamani 20 alipowatembelea katika ziara ya kushitukiza kwenye makazi yao yenye ulinzi mjini Roma. Papa Francis alizungumza na wanawake hao, ambao baadhi yao walisafirishwa kutoka Afrika na maeneo mengine ya Ulaya, kwa muda wa zaidi ya saa moja.
Pope Francis is given a rosary during his visit to the Papa Giovanni XXIII community in Rome, Friday, Aug. 12, 2016. Francis has met with 20 women from six countries who have been freed from prostitution as part of his Holy Year of Mercy activities focusing on communities that have experienced suffering. (L'Osservatore Romano/Pool Photo via AP)Wanawake hao waliokolewa kutoka kwenye madanguro walikokuwa wametekwa na mwanamume aliyekua akiwauza kama makahaba na sasa wamepewa makazi na ulinzi katika jengo la ghorofa linalomilikiwa na kanisa katoliki katika Mji Mkuu wa Italia.
Pope Franci, left, sits during his visit to the Papa Giovanni XXIII community in Rome, Friday, Aug. 12, 2016. Francis has met with 20 women from six countries who have been freed from prostitution as part of his Holy Year of Mercy activities focusing on communities that have experienced suffering. (L'Osservatore Romano/Pool Photo via AP)Papa Francis mwenye umri wa miaka 79 amekua akirejelea mara kwa mara kwamba biashara ya kuwasafirisha binadamu “ni uhalifu dhidi ya binadamu”.
Pope Francis kisses a baby during his visit to the Papa Giovanni XXIII community in Rome, Friday, Aug. 12, 2016. Francis has met with 20 women from six countries who have been freed from prostitution as part of his Holy Year of Mercy activities focusing on communities that have experienced suffering. (L'Osservatore Romano/Pool Photo via AP)Papa Francis aliketi na wanawake hao, wakiwemo wanaigeria saba, waromania sita na wanne kutoka Albania, na kusikiliza habari zao kuhusu namna walivyo lazimishwa ukahaba, ulisema utawala wa Vatican.
Pope Francis talks to a woman during his visit to the Papa Giovanni XXIII community in Rome, Friday, Aug. 12, 2016. Francis has met with 20 women from six countries who have been freed from prostitution as part of his Holy Year of Mercy activities focusing on communities that have experienced suffering. (L'Osservatore Romano/Pool Photo via AP)Wengine watatu katika kundi hilo wanatoka Italia, Tunisia na Ukraine.
Pope francis (2)Wote pamoja walikua na umri wa takriban miaka 30 na ”walinyanyaswa sana kimwili” na sasa wanaishi chini ya ulinzi, umesema uongozi wa Vatican.
Pope francis (3)Kwa ahadi za ajira, wanaofanya biashara ya kuwasafirisha binadamu huwaleta wanawake Italia na nchi nyingine za Ulaya magharibi , lakini baadae huwalazimisha kuingia ukahaba.
Pope francis (1)Papa Francis aliwatia moyo makahaba hao wa zamani “kuwa thabiti” wakati wanapoanza maisha mapya kwa usaidizi wa kituo cha Papa Pope John XXIII.

Comments

Popular posts from this blog