Mume, Mke Wachinjwa Kinyama.

waombolezaji wakiaga miili ya marehemu Majeneza yenye miili ya marehemu hao.
Na Gregory Nyankaira, RISASI MCHANGANYIKO
MARA: Hali mbaya! Wanandoa Said Somba (48) na Kadogo Ehijo (47), wakazi wa Kitongoji cha Rugala, Kijiji cha Mazami, Kata ya Bukabwa wilayani Butiama mkoani hapa wameuawa kwa kuchinjwa shingo na watu wasiojulikana, Risasi Jumatano lina kila kitu.
somaMarehemu Somba (kushoto) na marehemu Kadogo kulia.
Diwani wa Kata ya Bukabwa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kitongoji cha Rugala, Jonas Maswe aliliambia gazeti hili kuwa, tukio hilo lilijiri usiku wa Mei 25, mwaka huu ambapo watu hao wakiwa na mapanga walivamia nyumbani kwa Somba akiwa amelala na mkewe na kuwachinja.
baadhi ya watoto wa marehemu wakilia juu ya jeneza la baba yaoBaadhi ya watoto wa marehemu wakilia juu ya jeneza la baba yao
Alisema wakati wanachinjwa, wanandoa hao hawakupiga kelele na baada ya ukatili huo  wauaji hao waliifunika miili yao kitandani kisha wakatokomea kusikojulikana.
 Alisema mauaji hayo yalifanyika kimyakimya kwani hata  watoto wa marehemu waliokuwa wamelala nyumba ya pili hawakusikia lolote.
“Asubuhi ya saa 1 mtoto mmoja wa marehemu  aliamka, akaenda kuwaamsha wazazi wake ili wamfungulie mlango ajiandae kwenda shuleni.
“Mtoto huyo aliwaita wazazi wake mara kadhaa bila majibu hivyo aliusukuma mlango ambao ulikuwa umeegeshwa tu, akaingia ndani ya nyumba hiyo na alipoingia chumba cha wazazi wake aliwaona wamelala wakiwa wamejifunika shuka.
waombolezajiWaombolezaji wakiwa msibani.
“Aliwasalimia wakawa kimya, aliwashika na kukutana na  dimbwi la damu, akawaona wazazi wake wamefariki dunia huku wakiwa na majeraha makubwa shingoni.
“Yule mtoto alipiga kelele zilizowaita majirani nyumbani na kushuhudia unyama waliotendewa wanandoa hao,” alisema Maswe.
Mtoto mkubwa wa marehemu hao, Amos Said (26) alisema kwamba, licha ya kuwepo mifugo mingi  nyumbani hapo kama vile ng’ombe na mbuzi, lakini wauaji hao hawakuchukua mfugo hata mmoja.
Katibu wa Tarafa ya Makongoro, Khamis Waryoba, alilaani kitendo hicho na kuapa kusaidiana na Jeshi la Polisi Wilaya ya Butiama kuwasaka watu waliohusika katika unyama huo.
Polisi wilayani Butiama imethibitisha kuwepo kwa mauaji hayo na kusema kuwa, wanaendelea na msako mkali wa kuwabaini waliohusika.
Akizungumzia mauaji yanayoendelea, Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Musa, alikemea hali hiyo, akiwataka Watanzania kumuomba Mungu aepushe roho hizo za mauaji kwani hali siyo nzuri.
“Jamii lazima imuogope Mungu, pia kwa kushirikiana na vyombo vya usalama iwafichue wahalifu wanaotekeleza mauaji haya huku na sisi viongozi wa dini tukiendelea kuwaombea ili waachane na roho mbaya walizonazo kwani mambo kama haya hatujayazoea, tumekuwa tukiyaona kwenye nchi za wenzetu,” alisema kiongozi huyo, akiungwa mkono na mchungaji  wa kanisa moja la kiroho lililopo Madale, Koplo Jacob.
“Siyo jambo la kujivunia sana kuwa na jamii isiyoogopa mauaji, kila siku unaposikia watu wanauana ni hatari kwa taifa, sala maalum inahitajika ili kuwakomboa watu kifikra,” alisema.
Miili ya marehemu hao, ilizikwa Mei 26, mwaka huu, kwenye makaburi ya nyumbani kwao.
 Bwana alitoa na Bwana ametwaa, jina lake libarikiwe. Amina.

Comments

Popular posts from this blog