Muhammad Ali Kuzikwa Kishujaa Leo

muhammad aliii (2)Muhammad Ali
LOUISVILLE, Marekani
GWIJI wa ndondi duniani, Muhammad Ali, anatarajiwa kuingizwa kwenye nyumba yake ya milele kwa heshima kubwa leo Ijumaa baada ya sara maalum ya Kiislam huko Louisville, Kentucky, Marekani.
Muhammad Ali (2)Ratiba ya sara za mazishi, ilianza juzi Jumatano na jana zaidi ya watu 14,000 kuzikwa kishujaa leo waliungana kuomboleza kwa sala katika ibada iliyorushwa moja kwa moja kwenye televisheni.
Ali, alifariki dunia Ijumaa iliyopita akiwa na umri wa miaka 74 baada ya kusumbuliwa kwa muda mrefu na ugonjwa wa Parkinson ambao unashambulia mfumo wa seli. Mazishi yake leo yanatarajiwa kushirikisha wawakilishi kutoka dini mbalimbali wakiwemo Wayahudi na Wakristo.
Ali, alianza kupanga jinsi mazishi yake yatakavyokuwa mwaka mmoja uliopita na akasisitiza yawe huru kwa kila mmoja anayetaka kuhudhuria, afanye hivyo bure, familia imethibitisha. Ali ameacha mke na watoto tisa.

Comments

Popular posts from this blog