Tanzia: Aliyekuwa Mkurugenzi wa Jiji la Dar, Wilson Kabwe Afariki Dunia

kabwe 
Marehemu Wilson Kabwe.
ALIYEKUWA Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Wilson Kabwe amefariki usiku wa kuamkia leo nchini India alikokuwa ameenda kutibiwa. Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita amethibitisha kutokea kwa msiba huo.
Rais John Pombe Magufuli, Aprili 19 alimsimamisha kazi Bw. Wilson Kabwe kutokana na ufisadi katika utekelezwaji wa mikataba mitatu, inayohusu maeneo ya ukusanyaji mapato ya Stendi Kuu ya Mabasi Yaendayo Mikoani ya Ubungo na kodi ya uegeshaji magari katikati ya jiji na  kuisababishia  serikali  hasara  ya  pesa zaidi ya bilioni 3.
Rais Magufuli alichukukua uamuzi huo siku ya uzinduzi wa daraja la Kigamboni, ambapo kabla ya Rais kuhutubia, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,  Paul Makonda alitoa hotuba fupi ya maswala kadhaa ya Mkoa wa Dar es Salaam  ikiwemo  ripoti ya tume aliyounda  kuchunguza utekelezwaji wa mikataba hiyo.
Kabla ya kuhamishiwa jijini Dar es Salaam, Kabwe alikuwa ni Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza ambaye alihamishiwa Mwanza akitokea Mbeya baada ya kutuhumiwa kwa  ufisadi wa mabilioni kadhaa jijini humo.
Taarifa zisizo rasmi zinasemekana kuwa tangu siku ‘alipotumbuliwa’ na Rais Magufuli mbele ya halaiki ya watu, alipatwa mshtuko ambapo alipelekwa nchini India ili kupatiwa matibabu ambako mauti yamemkuta.

Comments

Popular posts from this blog