SHILOLE KWENYE PENZI LINGINE JIPYAA,KAHAMISHIA MAPENZI YAKE HAPAA!!



Kuvunjika kwa mahusiano na Nuh Mziwanda, taarifa za chini zimezidi kuenea kuwa Shilole ana mahusiano ya kimapenzi na msanii chipukizi wa Bongo Fleva, Nerd aliye chini ya label ya Ommy Dimpoz, PKP.

Akiongea kwenye kipindi cha Busati, kinachoruka kupitia Magic FM, Shilole amesema hana mpenzi kwa sasa.

“Mimi mpenzi wangu ni hela, Nerd ni rafiki yangu. Ukiwa kwenye mapenzi unakuwa kama kipofu unakuwa hauoni. Ukimkabidhi mtu moyo wako anakuwa anaufinyanga, kwa sasa moyo wangu umestawi tofauti na zamani,” aliongeza.

Shilole amesema hana namba ya Nuh Mziwanda na hajawahi kuwasiliana naye tangu walipoachana. Kwa sasa muimbaji huyo ana wimbo mpya uitwao Say My Name

Comments

Popular posts from this blog