Diamond na Kampuni yake ya Music WCB Yamzawadia Gari Jipya Harmonize


WCB imemzawadia gari jipya msanii wake, Harmonize.
Bosi wake, Diamond, ameandika kwenye Instagram: Kama nikusiivyo siku zote ni juhudi na nidhamu yako ndio itayokufanya upate matunda ya kazi yako….. Usiache unyenyekevu, kuheshimu mkubwa na mdogo, kumuomba na kumshukuru Mwenyez Mungu kwa kila hatua ndogo Uipigayo…. Congrats kwa your New Ride.”

Naye Harmonize hakuacha kuonesha furaha yake.

“Nichukue fursa fupi kuushukuru uongozi wangu mzima wa @wcb_wasafi @mkubwafella @babutale @sallam_sk @ricardomomo @diamondplatnumz kwa kunijali na kunithamini kijana wao wakanizawadia gari daaaaah furaha niliyo nayo haielezeki,” ameandika msanii huyo.

“Kwakweli nina furaha na ninashukuru sanaa nina mengi ya kuongea lakini sizani kama nikianza kuandika nitamaliza kubwa ni kwamba namshukuru m/mungu nashukuru kwa kurudia tena uongozi wangu @wcb_wasafi kwa zawadi lakini nitakuwa mchoyo wa fadhila nisipo washukuru wazazi wangu walio nizaa na kunilea hadi nikafikia hapa na shukrani za dhati ziwafikie mashabiki zangu ambao wapo bega kwa bega kunisupport katika kazi zangu pia mama naseeb umekuwa ukinisistiza na kunisihi jinsi ya kuishi na watu @kendrah_michael.”

“Nimalize kwakusema ninashukuru sanaa na nina amini kuna mengi mazuri zaidi yapo mbele ila asieshukuru na kidogo kamwe hatoshukuru na kikubwa thanks #allah thanks #wcb #thanks #mashabiki.”

Comments

Popular posts from this blog