WATU SABA AKIWAMO MTOTO WAUWAWA KWA RISASI MAREKANI

Watu saba wameuwawa kwa kupigwa risasu akiwemo mtoto wa miaka nane huku wengine kadhaa wakijeruhiwa katika tukio la mauaji lililotokea huko Kalamazoo, Michigan nchini Marekani jana usiku.
Mkuu wa Usalama wa Umma wa Kalamazoo Jeff Hadley mtuhumiwa wa mauaji hayo amekamatwa leo asubuhi.

Polisi wamesema mtuhumiwa huyo amekamatwa kwenye gari linaloshabihiana na lililotumiwa mshambuliaji, ambapo pia bunduki ilipatikana kwenye gari hilo.

Mtuhumiwa huyo mzungu mwanaume mwenye umri wa miaka 45, ni mkazi wa kaunti ya Kalamazoo, imeelezwa alijisalimisha bila ya purukushani.

Comments

Popular posts from this blog